“Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas amesema hayupo tayari kuliingiza Taifa kwenye njaa kwa kuendekeza wafugaji na kwamba ni marufuku wafugaji kuingia kwenye maeneo ya wakulima.Akizungumza na watumishi wa Halmashauri ya Madaba Wilaya ya Songea Kanali Thomas amesisitiza kuwa Mkoa wa Ruvuma sio Mkoa wa wafugaji bali ni Mkoa wa kilimo ambao unaongoza kitaifa kwa kuzalisha mazao ya chakula .
KATA ya Lituta Halmashauri ya Madaba Wilaya ya Songea Mkoani Ruvuma inatekeleza mradi wa sekondari mpya ya mfano kupitia mradi wa Kuboresha Elimu ya Sekondari nchini (SEQUIP)ambapo serikali kupitia mradi huo imetoa shilingi milioni 470.MKuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas amekagua mradi huu .Katika Mkoa wa Ruvuma zinajengwa shule za sekondari 11 kupitia mradi wa SEQUIP kwa gharama ya shilingi bilioni 7.7
WATUMISHI wa Ifinga Kata ya Matumbi Halmashauri ya Madaba Wilaya ya Songea mkoani Ruvuma walikuwa wanatumia nusu ya mshahara wao kwa safari pia wananchi walikuwa wanakodi pikipiki kwa shilingi 15,000 hadi eneo lenye mtandao wa simu ili kupiga simu,Akitoa historia ya kijiji cha Ifinga Kwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma.Mkuu wa Wilaya ya Songea Mheshimiwa Pololet Mgema amesema kijiji hicho tangu uhuru kilikuwa na changamoto nyingi ambazo sasa serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan imezipatia ufumbuzi wa kudumu.Amezitaja changamoto ambazo tayari zimetatuliwa kuwa ni matengenezo ya barabara,kuweka huduma ya Mawasiliano ya simu.kuweka huduma ya maji ya bomba na kuanza mradi wa ujenzi wa kituo cha Afya.Ifinga ni kijiji pekee mkoani Ruvuma ambacho kipo kilometa 48 toka barabara kuu ya Songea-Njombe ambacho kinaunda Kata ya Matumbi yenye kijiji kimoja cha Ifinga.
Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa