• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

UJENZI WA NYUMBA NNE ZA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MATETEREKA WAKAMILIKA

Posted on: August 12th, 2025

Ujenzi wa nyumba nne za walimu katika Shule ya Sekondari Matetereka, Halmashauri ya Wilaya ya Madaba, mkoani Ruvuma, umekamilika kwa mafanikio makubwa. Mradi huu umegharimu kiasi cha Shilingi Milioni 201 zilizotolewa kupitia Mradi wa Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) kwa mwaka wa fedha 2023/2024.

Akizungumza wakati wa kukagua nyumba hizo, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba, Wakili Sajidu Idrisa Mohamed, aliwapongeza viongozi wa kijiji pamoja na walimu kwa ushirikiano mzuri waliouonesha katika utekelezaji wa mradi huo muhimu.

Wakili Sajidu aliwahimiza walimu kuanza kuzitumia nyumba hizo mara moja, akisisitiza kuwa zinatatua changamoto ya makazi kwa walimu waliokuwa wakiishi mbali na shule. Alisisitiza umuhimu wa kuzitunza nyumba hizo ili ziweze kudumu na kutoa huduma bora kwa muda mrefu.

Kwa upande wao, uongozi wa Shule ya Sekondari Matetereka umeishukuru Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa kutoa fedha zilizowezesha ujenzi huo. Wameeleza kuwa nyumba hizo zitaboresha mazingira ya kazi kwa walimu na hivyo kuinua kiwango cha taaluma shuleni hapo.

Mradi huu ni sehemu ya jitihada za serikali katika kuboresha mazingira ya kufundishia na kujifunzia nchini, hasa katika maeneo ya vijijini.

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • UHISHWAJI WA BARAZA LA WAZEE MADABA WAFANYIKA LITUTA.

    November 22, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MADABA YAPEWA CHETI CHA PONGEZI KWA UTEKELEZAJI BORA WA LISHE

    November 21, 2025
  • TIMU YA UKAGUZI MKOA WA RUVUMA YAFURAHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MADABA.

    November 08, 2025
  • TIMU YA UKAGUZI KUTOKA MKOANI YATUA MADABA KWA UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO.

    November 06, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa