Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Madaba Wilaya ya Songea mkoani Ruvuma Sajidu Idrisa Mohamed amesema kampuni mbili za uchimbaji madini ya makaa ya mawe zinatarajia kuanza kuchimba madini hayo katika kata za Mtyangimbole na Gumbiro kuanzia mwezi Machi mwaka huu.Sajidu ametoa taarifa hiyo wakati anazungumza kwenye mkutano wa Baraza la madiwani la Halmashauri hiyo mjini Madaba
MKuu wa Wilaya ya Songea Mhe, Pololet Mgema ameseam Halmashauri ya Madaba ilishajowekea utaratibu wa kila mwezi kupanda miti kwa lengo la kendelea ya kutunza vyanzo vya maji pamoja na mazingira kwa ujumla.Hayo ameyasema jana januari 20, 2023 katika kikao cha robo ya pili ya mwaka cha baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Madaba wilaya ya Songea kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri hiyo
Mkuu wa Wilaya ya Songea Mheshimiwa Pololet Mgema amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Madaba kwa kushirikiana na watendaji wa kata kuanza msako wa nyumba kwa nyumba kuwatafuta wanafunzi wa sekondari ambao hadi sasa hawajaripoti katika shule walizopangiwa Akizungumza kwenye mkutano wa Baraza la madiwani Halmashauri ya Madaba Mheshimiwa Mgema ameagiza hadi kufikia mwishoni mwa Januari mwaka huu wanafunzi wote wawe shuleni.Awali akitoa taarifa ya mahudhurio ya wanafunzi wa sekondari,Afisa Elimu Sekondari Maternus Ndumbaro amewataja jumla ya wanafunzi 1269 walipangwa katika shule za sekondari kuanza kidato cha kwanza ambapo hadi kufikia Januari 19,2023 ni wanafunzi 535 ndiyo wameripoti sawa na asilimia 42 ambapo asilimia 58 ya wanafunzi bado hawajaripoti.
Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa