• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

ZAIDI ya Shilingi Milioni 600 za Mradi wa Boost kujenga miundombinu ya Shule ya Msingi na awali Madaba

Posted on: April 24th, 2023

Halmashauri ya Madaba wameanza utekelezaji wa mradi wa Boost unaotekelezwa kwa zaidi ya shilingi Milioni 600 katika mwaka wa fedha 2022/2023.

Timu ya wataalamu wa Halamshauri hiyo imetembelea Kata ya Mahanje ambayo katika mradi huo wamepewa Shule 2 ya Mahanje na Ifugwa.

Afisa Elimu Msingi Vifaa na takwimu Raphael Kibiligi wa Halmashauri hiyo amesema kwa awamu ya kwanza ya mradi wamepewa shule 6 kati ya shule 28 timu hiyo yenye wataalamu 12 imeanza  kutamburisha mradi  kwa wananchi wa Kata ya Mahanje.

Hata hivyo amesema Shule ya Msingi Mahanje imepewa ujenzi wa vyumba  2 vya Madarasa  yenye thamani ya shilingi Milioni 48,000,000/= na matundu ya vyoo 3 yenye thamani ya Shilingi milioni 5,100,000/= jumla katika Shule hiyo Milioni 53,100,000/=.

Katika Shule ya Msingi Ifugwa wamepewa zaidi ya  shilingi milioni 66 kwaajili ya ujenzi wa madarasa 2 ya awali ya mfano na matundu ya vyoo 6 ikiwa vyoo 2 vya walemavu na vyoo vinne vya kawaida.

Kaimu Mwenyekiti wa timu hiyo Afisa Maendeleo ya Jamii Bashiru Mgwasa akizungumza na hadhara katika Kata ya Mahanje amesema majukumu ya wananchi ikiwa ni pamoja na kutambua mradi na fedha zilitengwa kwaajili ya ujenzi wa miundombinu ya Shule,Kuandaa eneo la ujenzi na kuhakikisha eneo hilo halina migogoro.

Amesema wananchi wajibu wao ni pamoja na kuchimba mashimo ya vyoo,kusafisha eneo la ujenzi pamoja na kuchimba msingi wakati wa ujenzi.

Diwani wa Kata ya Mahanje Stephano Mahundi akizungumza na wananchi hao ametoa rai kwa wananchi hao kuhakikisha wanasimamia miradi hiyo kwa weledi na kutoa taarifa kwa viongozi kwa wale watakaoenda kinyume na matakwa ya Serikali.

“Mradi huu umekuja kwaajili ya sisi wanamahanje naomba kwa vile umekuja kwetu haijawahi kutokea darasa kujengwa kwa shilingi milioni 24 na Madarasa haya  ya mfano tuhakikishe tunasimamia kwa nidhamu ya hali ya juu sana”.

Hivyo Mahundi amewasihi wananchi kuwa na umoja mara baada watakapoambiwa kusafisha eneo,kuchimba msingi baada ya hapo utaratibu utaendelea kwaajili ya ujenzi na kuhakikisha usimamizi wa ujenzi huo upo mikononi mwa wananchi.

Kutoka Halmashauri ya Madaba

Aprili 24,2023.

 

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Chwaya atoa rai kwa walimu wa awali kutekeleza agizo la Serikali

    January 18, 2025
  • MARATIBU wa mradi wa BOOST Madaba amshukuru Rais Samia

    January 18, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa