• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Muundo wa Utawala
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika

WAZIRI wa Maji awaomba wakuu wa Mikoa kusimamia miradi ya maji

Posted on: July 6th, 2021

Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso (Mb) amewaomba Wakuu wa mikoa na Makatibu Tawala wa mikoa kushirikiana katika usimamizi wa miradi ya maji nchini.


Mhe. Aweso amesema hayo katika kikao cha mafunzo ya uongozi kwa Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala wa Mikoa ya Tanzania Bara kinachofanyika jijini Dodoma.


Amesema Wizara ya Maji imedhamiria kuhakikisha lengo la kumtua mama ndoo ya maji linafikiwa kama lilivyoelekezwa na serikali.

"Niwaombe viongozi tushirikiane kwa dhati kuhakikisha tunaondoa changamoto zote za upatikanaji wa huduma ya majisafi. Peke yetu hatutaweza." Aweso amesema.


Pamoja na hilo amepokea mapendekezo mbalimbali kutoka kwa viongozi hao wa mikoa na kuwaahidi kuyafanyia kazi.


“Kuhusu kuwa na utaratibu wa wadau wa maji kukutana na kujadili masuala mbalimbali yanayohusiana na sekta ya maji ni jema sana.

Naomba nipokee ushauri wenu wa jinsi ya kulitekeleza ili liwe endelevu. Isiwe ni maelekezo ambayo yanaweza kubadilishwa na kiongozi mwingine. Liwe ni muongozo rasmi na utamaduni ili hata kiongozi ajaye, afanye hivyohivyo" Aweso amesema.


Amesisitiza kuwa Wizara ya Maji haitakuwa kikwazo katika kufikia malengo. Amezitaja baadhi ya hatua zilizochukuliwa na Wizara ili kuimarisha usimamizi wa miradi ya maji kuwa ni pamoja na uamuzi wa kuingia makubaliano na Chuo cha Maji ili kuwatumia wahitimu wa chuo hicho katika usimamizi na uendeshaji wa miradi ya maji nchini.


Wakuu hao wa mikoa na Makatibu Tawala wa Mikoa ya Tanzania Bara wanashiriki mafunzo ya uongozi Jijini Dodoma.

Imeandikwa na Afisa Habari Wizara ya Maji Dodoma

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • TANGAZO LA AJIRA ZA SENSA May 05, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 10, 2021
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • MAAFISA Ugani 34 Ruvuma wapatiwa mafunzo ya upimaji wa afya ya udongo

    May 20, 2022
  • MKOA wa Ruvuma watoa chanjo ya polio kwa asilimia 122

    May 20, 2022
  • HALMASHAURI ya Madaba yaazimia kukamilisha miradi kabla ya mwaka wa fedha 2021-2022 kuisha

    May 19, 2022
  • IBUGE azitaka Halmashauri kutoa Mikopo ya asilimia 10 kwa Vikundi vya TASAF

    May 15, 2022
  • Angalia zote

Video

RUVUMA HAINA SHULE YA LITEPATILE,TAARIFA ZILIZOTOLEWA NI UZUSHI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 10

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: info@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa