• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

WATUMISHI Ruvuma walia na mishahara midogo

Posted on: May 2nd, 2021

WAFANYAKAZI mkoani Ruvuma wamelalamikia mishahara yao kuwa bado ni midogo ukilinganisha na hali halisi ya maisha ya wafanyakazi.

Akisoma risala ya wafanyakazi wa Mkoa wa Ruvuma katika sherehe ya Mei Mosi iliyofanyika kimkoa mjini Mbambabay wilayani Nyasa,Katibu wa TUGHE Mkoa wa Ruvuma Ismail Mudathir amesema katika sekta ya umma na binafsi mishahara haikidhi mahitaji ukilinganisha na kupanda kwa gharama za maisha.

“Tunaiomba serikali kupitia Mei Mosi hii,kwa itutazame jicho la kipekee kabisa iongeze mishahara na kuboresha maslahi kwa wafanyakazi kwa sababu ni muda mrefu sana mishahara haijaongezwa’’,alisisitiza Katibu wa TUGHE.Amesema watumishi wa Mkoa wa Ruvuma,wanakabiliwa na changamoto za kiutumishi zikiwemo baadhi ya waajiri kutowatendea haki baadhi ya watumishi hali ambayo ina punguza molali kwa wafanyakazi.

Amezitaja baadhi ya changamoto hizo kuwa ni kutolipwa madeni ya uhamisho wa watumishi,baadhi ya watumishi kutopandishwa madaraja kwa wakati na baadhi ya waajiri kutolipa nauli za watumishi na mizigo yao wanapostaafu.

Hata hivyo licha ya changamoto hizo Katibu huyo wa TUGHE kwa niaba ya watumishi mkoani Ruvuma amesema,wafanyakazi wanaahidi kuendelea kufanya kazi kwa bidii kwa maslahi mapana ya nchi ya Tanzania.

Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Nyasa Isabela Chilumba ametoa rai kwa watumishi kuwa na subira kwa sababu serikali ya Awamu ya sita imedhamiria kuboresha maslahi ya watumishi.

“Serikali mwezi huu imeanza kutoa barua za kuwapandisha madaraja watumishi wa umma wanaostahili katika nchi nzima na katika Halmashauri za wilaya baadhi ya watumishi wameanza kupata barua za kupandishwa madaraja kupitia maafisa utumishi’’,alisema Chilumba.

Hata hivyo amewaagiza waajiri kuhakikisha wanawalipa mafao na haki zao zote watumishi wanaostaafu na kuwaagiza waajiri kwenye Halmashauri na Taasisi zote za serikali kuacha kuchelewesha fedha za malipo ya likizo kwa watumishi wanaokwenda likizo.

Mei Mosi ni siku ya wafanyakazi wote duniani inayoadhimishwa kila mwaka ifikapo Mei Mosi,kauli mbiu ya mwaka huu ni maslahi bora,mishahara juu,kazi iendelee.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Tarehe 2/5/2021

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Chwaya atoa rai kwa walimu wa awali kutekeleza agizo la Serikali

    January 18, 2025
  • MARATIBU wa mradi wa BOOST Madaba amshukuru Rais Samia

    January 18, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa