• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

WATUMISHI Halmashauri ya Madaba waadhimisha Muungano kwa kusafisha Kituo cha Afya

Posted on: April 26th, 2022

HALMASHAURI ya Madaba Wilaya ya Songea imeadhimisha Muungano wa miaka 58 kwa kufanya Usafi wa Mazingira  maeneo ya Kituo cha Afya.

Akizungumza Mkurugenzi  Mtendaji wa Halmashauri hiyo Sajidu Idrisa Mohamed mara baada ya zoezi hilo amesema Sikukuu hiyo  itaendelea kuwa alama ya mafanikio ya Muungano katika nchi ya Tanzania  na Zanzibar pamoja na kuwaenzi Viongozi ambao ndio waasisi wa Taifa la Tanzania.

“Tudumishe Muungano kama ambavyo tulivyojumuika kwa pamoja  sisi  wananchi wa Halmashauri ya Madaba  kwa kuunga Juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani,tukishirikiana na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma kuhimiza wananchi kuweka mazingira katika hali ya Usafi”.

Mganga Mkuu wa Halmashauri hiyo Mussa Rashid amewapongeza wanafunzi kutoka Shule ya Madaba Day pamoja na Mahanje kwa kusherekea sikukuu ya Muungano kwa kuweka Mazingira safi  na kumuunga Mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

“Na hii inaonyesha kwa jinsi gani tunavyomuunga Mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Rais Samia Suluhu Hassan,leo ni siku muhimu katika Taifa letu na tunawaenzi viongozi wasisi wa Taifa letu Nchi imekuwa na Umoja”.

Hata hivyo Mganga Mkuu amewasa Wanafunzi hao kuendelea kuwa wazalendo kupitia kazi kubwa waliyofanya leo kwa kuweka mazingira katika hali ya usafi na  hata watakapokuwa watumishi mara baada ya kuhitimu masomo yao wakaendelee kuwa na moyo wa uzalendo.

“Moyo wa uzalendo usiishie leo tunatarajia kuwaona mnasoma kwa bidii, mkiwa na nidhamu ya hali ya juu na tunatarajia kuwaona mnachapa kazi kwa bidii”.

Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya Madaba Anita Makota amesema katika zoezi hilo la usafi katika siku ya Muungano limekuwa jambo jema kwanza ni  mazoezi na kuendeleza kazi pamoja na kuleta maendeleo na mshikamano.

Kwa upande wake Mwanafunzi wa Shule ya Sekondari Madaba Day Saimon Emanuel amesema zoezi hilo la kufanya Usafi katika kituo cha afya , kwanza limesaidia kuwaweka kwa pamoja na viongozi wa Halmashauri hiyo pamoja na kuyaenzi yale ambayo viongozi wa Taifa walianzisha.

Imeandaliwa na Aneth Ndonde

April 26,2022

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • UJENZI WA MADARASA 2 NA MATUNDU 6 YA VYOO SHULE YA MSINGI KIPINGO WAKAMILIKA KWA ASILIMIA 100

    May 30, 2025
  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Chwaya atoa rai kwa walimu wa awali kutekeleza agizo la Serikali

    January 18, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa