• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

WATENDAJI Mkatekeleze majukumu yenu Serikali ya awamu ya sita imewaona

Posted on: March 2nd, 2023

MWENYEKITI wa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba Teofanes Mlelwa amewakabidhi pikipiki 6  watendaji wa Kata.

Akizungumza katika zoezi hilo lililofanyika katika Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo amempongeza Rais wa awamu ya Sita Samia Suluhu Hassan kwa kuwaona Watendaji Kata na kuwapa pikipiki ambazo zitarahisisha kutekeleza majukumu yao kwa wakati.

“Sitegemei kuona Mtendaji hajui majukumu yake Rais Samia amewaona kuwa mna kata,vijiji,Mitaa pamoja na vitongoji hivyo mkahakikishe mnatembelea miradi yote ya maendeleo”.

Hata hivyo Mlelwa amewaasa watendaji  hao kutumia pikipiki hizo kwa matumizi sahihi na kuepuka kutumia katika mambo yao binafsi.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashari hiyo Sajidu Idrisa Mohamed kupitia zoezi hilo amesema  watendaji walikuwa wanapata changamoto kwa kutembea kwa umbali wa kilomita 120 kwa kata ya Mtyangimbole na Kata ya Matumbi kilomita 48 kuja Halmashauri wanapohitajika.

“Kupitia hizi pikipiki tulizotoa hatuhitaji kusikia visingizio vya kuchelewesha taarifa na kuripoti miradi inayoendelea katika Kata zenu”.

Hata hivyo Mohamed amesema kutokana na changamoto ambazo zilikuwa zimewapata Watendaji kwa mda mrefu Serikali ya awamu ya Sita  imeona uhumimu na kuwapatia pikipiki 6  kwa Kata za Halmashauri ya Madaba ili kuondoa changamoto hizo.

Mohamed ametoa shukrani za dhati kwa Dkt Samia Suluhu Hassan  kwa kuwaongezea Watendaji  ufanisi katika kazi na kurahisisha  usafiri  katika utekelezaji wa majukumu ya kazi.

“Napenda kuchukua fursa hii kuwataka Watendaji wote wa Kata mliopewa pikipiki hizi kuhakikisha mnazitunza sawa na malengo yaliyokusudiwa pamoja na kuhakikisha mnazifanyia matengenezo ya mara kwa mara”.

Imeandaliwa na Aneth Ndonde

Kutoka Kitengo cha Mawasiliano Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Madaba

Machi 2,2023.

 

 

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MADABA YAPONGEZWA KWA KUPATA HATI SAFI KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    June 19, 2025
  • UJENZI WA MADARASA 2 NA MATUNDU 6 YA VYOO SHULE YA MSINGI KIPINGO WAKAMILIKA KWA ASILIMIA 100

    May 30, 2025
  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa