• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

VIONGOZI Madaba wamshukuru Rais Samia kwa kuleta fedha za maendeleo

Posted on: July 28th, 2023

MWENYEKITI wa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba Teofanes Mlelwa ametoa rai kwa Waheshimiwa Madiwani kusimamia miradi ya Maendeleo katika Kata zao.

Hayo amesema katika Kikao cha Baraza la Madiwa cha robo ya nne ya Mwaka wa Fedha 2022/2023 kilichofanyika katika ukumbi wa ofisi ya Mkurugenzi na kuwapongeza wataalam kwa kusimamia miradi ya maendeleo.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba Sajidu Idrisa Mohamed ametoa rai kwa Waheshimiwa Madiwa kutoa ushirikiano wa kusimamia miradi ya maendeleo inayoletwa na Rais Samia.

 “Katika Mwaka huu wa Fedha tunaoanza tunaomba ushirikiano uleule tulioonyesha mwaka wa fedha 2022/2023 tuonyeshe ushirikiano pia katika mwaka mpya wa fedha 2023/2024 pamoja na kuhamasisha wananchi waweze kuipokea miradi ambayo Rais anatulete ”.

Hata hivyo Mkurugenzi amewashukuru  wataalam wa Halmashauri hiyo kwa usimamizi wa miradi na kuwaomba kuendelea kushirikiana na waheshimiwa madiwani kwa umoja wa kusimamia miradi hiyo itakayotekelezwa Mwaka mpya wa Fedha 2023/2024.

“Shukrani za pekee zimwendee Mh.Rais Samia kupitia Mbunge wetu Joseph Mhagama akitusemea huko Bungeni pamoja na ninyi waheshimiwa Madiwani”.

Hata hivyo amesema mwaka wa fedha 2022/2023 zimepokelewa fedha kiasi cha zaidi ya shilingi bilioni moja kwaajili ya ujenzi wa Madarasa na Shule moja mpya .

Mohamed amewaomba Waheshimiwa Madiwani kuisemea miradi hiyo kwa wananchi ili wajue juhudi  Rais Samia zinazofanyika katika Halmashauri ya Wilaya ya Madaba kila wanapofanya mikutano  katika Kata zao.

Imeandaliwa na Aneth Ndonde

Kutoka Kitengo cha Mawasiliano Halmashauri ya Madaba

Julai 28,2023.

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • UJENZI WA MADARASA 2 NA MATUNDU 6 YA VYOO SHULE YA MSINGI KIPINGO WAKAMILIKA KWA ASILIMIA 100

    May 30, 2025
  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Chwaya atoa rai kwa walimu wa awali kutekeleza agizo la Serikali

    January 18, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa