Ujenzi wa vyumba viwili (2) vya madarasa na matundu sita (6) ya vyoo katika Shule ya Msingi Kipingo iliyopo kata ya Lituta, Halmashauri ya Wilaya ya Madaba, umekamilika kwa asilimia 100.
Mradi huu umegharimu kiasi cha Shilingi Milioni 70.1 zilizotolewa kupitia Mradi wa BOOST unaotekelezwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa lengo la kuboresha miundombinu ya elimu ya awali na msingi nchini.
Kukamilika kwa ujenzi huu kunakwenda kupunguza changamoto ya uhaba wa madarasa katika shule hiyo na hivyo kuwezesha wanafunzi wa darasa la awali kupata mazingira bora ya kujisomea na kujifunzia kwa ufanisi zaidi.
Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, imeendelea kuonesha dhamira thabiti ya kuimarisha sekta ya elimu nchini kwa kutoa fedha kwa ajili ya uboreshaji wa miundombinu ya shule mbalimbali, ikiwemo Shule ya Msingi Kipingo.
Halmashauri ya Wilaya ya Madaba inatoa shukrani za dhati kwa mchango mkubwa wa Serikali katika kuhakikisha wanafunzi wanapata mazingira bora ya kusomea, jambo linaloendana na azma ya Serikali ya kuleta maendeleo ya kweli kupitia elimu bora kwa wote.
MADABA - RUVUMA
Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA
Simu: 0252951052
Simu ya Mkononi:
Barua pepe: ded@madabadc.go.tz
Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa