• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

TFS wapiga jeki taasisi za Kidini na Serikali

Posted on: July 20th, 2024

WAKALA wa  misitu Tanzania (TFS) kupitia shamba la miti Wino lililopo Halmashauri ya Wilaya ya Madaba wametoa msaada wa vifaa vya kukamilisha majengo katika taasisi za kidini na Serikali zikiwemo shule za Msingi na Sekondari pamoja na Zahanati zenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 39.

Mhifadhi Mkuu wa Shamba la miti wino Grory Fotunatus amekabidhi vifaa hivyo kwa Mbunge wa Jimbo la Madaba Mhe.Joseph Mhagama vikiwemo vifaa vya kanisa la Luthelani ushirika wa Lilondo wametoa nondo rolo 50 na saruji mifuko 100 yenye tahamani ya shilingi milioni 3,325,000/=.

Amesema parokia ya mtakatifu mama wa Mungu Lilondo wametoa mifuko 100 ya saruji sawa na shilingi 1,850,000/=,Kanisa jipya kigango cha matetereka mifuko 200 ya saruji sawa na shilingi Milioni 3,700,000/=,Kanisa la mtakatifu Agustino Madaba mifuko 100 ya saruji sawa na shilingi 1,850,000/=,Sekondari ya Wilma mifuko 200 ya saruji sawa na shilingi milioni 3,700,000/=,zahanati ya Mkongotema mifuko  200 sawa na shilingi milioni 3,700,000/=

Hata hivyo amesema sekondari ya Wino imepata vifaa vya ukarabati wa jengo la utawala thamani yake ni milioni 3,419,000/=,Sekondari ya Madaba mbao,nondo zenye thamani ya shilingi milioni 6,668,000/=,Sekondari ya Mahanje madirisha ya aluminium na vifaa vingine sawa na shilingi milioni 6,216,000/=,Shule ya Msingi Mkwera misumari,nondo,saruji na mabati jumla ya shilingi milioni 5,564,000/=

Mhagama amempongeza muhifadhi Mkuu wa shamba la Miti Wino kwa uhifadhi ambao wanamadaba wananufaika na uhifadhi huo.

“Uhifadhi huu umetunufaisha wanamadaba wote kwa namna moja au nyingine kila kijiji,shule ya msingi,sekondari ambao waliomba msaada TFS wakakosa tunamshukuru muhifadhi mkuu wa Taifa,Mhe.Waziri wa Wizara ya Maliasili na Utalii kwa namna ambavyo mmetujali wanamadaba”.

Imeandaliwa na Aneth Ndonde

Kutoka Kitengo cha Mawasiliano Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

Julai 18,2024.

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Chwaya atoa rai kwa walimu wa awali kutekeleza agizo la Serikali

    January 18, 2025
  • MARATIBU wa mradi wa BOOST Madaba amshukuru Rais Samia

    January 18, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa