• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Muundo wa Utawala
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika

TFS wakabidhi mifuko 150 ya Saluji kwa DC Ndile kwaajili ya ujenzi wa kituo cha Afya Ifinga

Posted on: June 3rd, 2023

MENEJA wa Wakala wa Misitu Shamba la Wino Grory Kassmir amekabidhi mifuko ya Saluji 150 yenye thamani ya shilingi milioni 2,475,000/=kwa Mkuu wa Wilaya ya Songea  Wilman Ndile.

Zoezi hilo limefanyika katika kijiji cha Ifinga amesema  kwaajili ya kuongeza nguvu ya ujenzi wa Kituo cha Afya Ifinga Halmashauri ya Madaba  fedha hizo zimetolewa katika mfuko wa mama Samia kupitia Wakala wa misitu  Tanzania.

“Sisi sote ni serikali tukaona  tuchangie kijiji cha ifinga tuendelee kuleta chachu ya kuongeza maendeleo ili kuhakikisha Ifinga inaendelea kuwa juu na tutaendelea kushirikiana kwa pamoja tunamsaidia Rais kwa pamoja”.

Hata hivyo Meneja ametoa rai kwa wananchi wa Ifinga kuendelea kutunza misitu na kuhakikishe hakuna moto unaotokea kwenye misitu  pamoja na kufuata  taratibu za kilimo cha mabonde na milimani.

“Najua sisi tunategemea kilimo cha mabondeni na milimani tuhakikishe tunalima kilimo rafiki tujue kilimo kinaweza kuhatarisha vyanzo vya maji au moto”

Amesema kuna kikosi maalumu ambacho kinaanza kazi kuanzia mwezi wa saba mpaka mwezi wa 12 kikosi cha moto na safari hii kutakuwa na mgambo ambao watapewa ajira ya moja kwa moja kwa wale watakao kidhi vigezo na watalipwa 260,000/=. Kwa mda wa miezi sita.

Mkuu wa Wilaya akipokea Saluji hiyo amewashukuru Wakala wa  Misitu Tanzania (TFS) shamba la Wino ambalo lipo katika Halmashauri ya Madaba

“Tunashukuru sana kwa mifuko ya saluji 150 imetolewa kwaajili ya kuwasaidia wananchi wa Madaba ambao wanaoishi kijiji cha Ifinga na maalumu kwaajili ya ujenzi wa kituo cha Afya maana mmewapa heshima wananchi wa kijiji cha hiki asanteni”.

Hata hivyo boma la kituo hicho limejengwa kwa shilingi Milioni 31,000,000/= fedha kutoka mapato ya ndani ya Halmashauri.

Kutoa kitengo cha Mawasiliano Halmashauri ya Madaba

Juni 3,2023.

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • RAIS Samia atoa Milioni 90 ukarabati wa Madarasa 6 Ifinga

    September 24, 2023
  • MWENYEKITI Madaba aagiza kuezeka Kituo cha Afya Ifinga Mara Moja

    September 24, 2023
  • WANANCHI Lilondo wajitolea kujenga Nyumba 6 za walimu

    September 23, 2023
  • WANANCHI Ifinga walivyojiwekea benki tofari 400,000 kwaajili ya Ujenzi wa Miradi ya Serikali

    September 23, 2023
  • Angalia zote

Video

MADIWANI MADABA WAADHIMIA KUSIMAMIA MIRADI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 10

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: info@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa