• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

SIKU YA KIMATAIFA YA MTOTO WA KIKE YAADHIMISHWA MADABA

Posted on: October 22nd, 2025

Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Mtoto wa Kike yamefanyika katika ukumbi wa Shule ya Sekondari Madaba, Wilaya ya Madaba mkoani Ruvuma, yakienda sambamba na kaulimbiu ya mwaka 2025 isemayo “Mimi ni msichana, kinara wa mabadiliko kwa Tanzania tuitakayo 2050.”

Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo alikuwa Afisa Maendeleo ya Jamii kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Bi. Mariam Juma, ambaye aliwataka wazazi, walezi na jamii kwa ujumla kuwekeza katika elimu, afya na ustawi wa mtoto wa kike ili kumwezesha kuwa kiongozi wa mabadiliko chanya kwa taifa la kesho.

Bi. Mariam alisema maadhimisho hayo ni sehemu ya kutambua changamoto mbalimbali zinazowakabili watoto wa kike, ikiwemo ukosefu wa elimu bora, mimba za utotoni, ukatili wa kijinsia na ukosefu wa fursa za kiuchumi, hivyo jamii inapaswa kushirikiana kuhakikisha wasichana wanapata haki na nafasi sawa na wavulana.

Sherehe hizo zilipambwa na burudani mbalimbali ikiwemo maigizo, ngonjera, mashairi na maonesho ya mitindo ya mavazi, yaliyobeba jumbe za kumtia moyo mtoto wa kike kuwa jasiri na mwenye ndoto kubwa.

Katika kuunga mkono juhudi za kumjengea mtoto wa kike mazingira salama ya kujifunza, Benki ya NMB ilishiriki kwa kutoa mchango wa taulo za kike, ikiwa ni ishara ya kuthamini na kujali afya ya mtoto wa kike.

Maadhimisho haya hufanyika kila mwaka ifikapo tarehe 11 Oktoba, kufuatia tamko la Umoja wa Mataifa namba 66 la tarehe 19 Desemba 2011, lenye lengo la kutambua na kushughulikia changamoto zinazowakabili watoto wa kike duniani.

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • UHISHWAJI WA BARAZA LA WAZEE MADABA WAFANYIKA LITUTA.

    November 22, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MADABA YAPEWA CHETI CHA PONGEZI KWA UTEKELEZAJI BORA WA LISHE

    November 21, 2025
  • TIMU YA UKAGUZI MKOA WA RUVUMA YAFURAHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MADABA.

    November 08, 2025
  • TIMU YA UKAGUZI KUTOKA MKOANI YATUA MADABA KWA UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO.

    November 06, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa