• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

SERIKALI yawapunguzia Wananchi umbali mrefu kufuata huduma za Afya Mahanje Madaba

Posted on: November 23rd, 2023

MKURUGENZI Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Madaba Sajidu Idrisa Mohamed ametoa rai kwa wananchi wa Kata ya Mahanje kuanza ujenzi wa Nyumba ya Mganga kwa nguvu za Wananchi.

Hayo amesema alipozungumza na wananchi hao walipo kabidhi Zahanati kwa wananchi iliyokamilika na  kuanza kutoa huduma ikiwa mwaka wa fedha 2024/2025 Halmashauri itatenga fedha kwaajili ya umaliziaji wa Nyumba hizo.

“Niwahakikishie tutaitengea  bajeti na kuweka vipaumbele vya upatikanaji wa fedha za umaliziaji wa Nyumba hizo pia iweze kupata ruzuku Serikalini”.

Hata hivyo Mkurugenzi amempongeza Meneja wa Tanesco Mkoa wa Ruvuma kwa kuhakikisha analeta Umeme katika Zahanati hiyo.

 Diwani wa Kata hiyo Stephano mahundi ameipongeza Serikali kwa kutoa fedha za ujenzi wa Zahanati hiyo pamoja na Mbunge wa Jimbo la Madaba Joseph Mhagama kwa kuhakikisha Zahanati hiyo inakamilika.

Naye Katibu mwenezi wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Songea Modesta Luoga ametoa rai kwa wananchi wa Mahanje kuhakikisha wanatunza Miundombinu ya Zahanati hiyo ili waweze kujipatia huduma kwa urahisi.

Kwa upande wake katibu wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Songea Juma Nambaila katika zoezi  hilo amesema Serikali ya Chama cha Mapinduzi imetoa huduma nyingi kwa Wananchi ikiwemo Afya,elimu, Maji na umeme.

“Kwetu sisi Chama ni Faida kubwa maana tulisimama kwenye majukwaa,tukaahidi na leo tumetekeleza sisi kama chama juhudi zetu ni kusukuma Serikali na wananchi ni wanufanika wa utekelezaji wa Ilani”.

Kutoka Kitengo cha Mawasiliano Halmashauri ya Madaba

Novemba 22,2023.

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Chwaya atoa rai kwa walimu wa awali kutekeleza agizo la Serikali

    January 18, 2025
  • MARATIBU wa mradi wa BOOST Madaba amshukuru Rais Samia

    January 18, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa