• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

OPARESHENI kabambe ya kuwaondoa waliovamia vyanzo vya Maji Mkoani Ruvuma

Posted on: February 1st, 2021

KIKAO cha wadau wa maji mkoani Ruvuma kilichoongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma kimeptisha azimio la kufanya operesheni kabambe ya kuwaondoa wote waliovamia kwenye vyanzo vya maji na kusababisha athari za kimazingira.

Mwenyekiti wa Kikao hicho ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme anasisitiza kuwa kwa wale ambao wameshalima kwenye vyanzo vya maji na mimea ishaota,msimu huu ni  mwisho,

“Tutaendesha operesheni ya kuwaondoa wale wote ambao wanakwenda kulima kwenye vyanzo vya maji na kusababisha watu wengine wapate maji machafu,hili halikubaliki lazima waondoke’’,anasisitiza Mndeme.

Anatoa rai kwa wenyeviti wa Halmashauri zote nane zilizopo katika Mkoa wa Ruvuma kuhakikisha kuwa suala la kuwaondoa waliovamia vyanzo vya maji linakuwa azimio kwenye vikao vya Baraza la madiwani.

Hata hivyo anasema kwa kuwa hivi sasa waliolima mahindi kwenye vyanzo vya maji,mahindi yamerefuka na tayari wameshaweka mbolea hivyo serikali haiwezi kwenda kung’oa katika msimu huu.

Ametahadharisha kuwa kilimo kwenye vyanzo vya maji kwa kutumia mbolea za kemikali kinaleta madhara makubwa kwa mtumiaji wa maji hayo ambaye anakunywa maji yenye mbolea hali ambayo inaweza kuleta athari za kiafya.

Kutokana na hali hiyo Mndeme amewaomba wadau wote wa maji kutoa elimu ya athari za  kuvamia vyanzo vya maji ambapo amesisitiza kuanzia mwakani mtu yeyote ambaye atafanya shughuli za kiuchumi kwenye vyanzo vya maji atachukuliwa hatua kulingana na sheria ya mazingira ya mwaka 2004 na sheria ya maji ya mwaka 2002 na 2019.

Imeandikwa na Albano Midelo

Februari Mosi,2021

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Chwaya atoa rai kwa walimu wa awali kutekeleza agizo la Serikali

    January 18, 2025
  • MARATIBU wa mradi wa BOOST Madaba amshukuru Rais Samia

    January 18, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa