• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

NAIBU Waziri wa Maji apiga marufuku kufanya shughuli za kibinadamu kwenye vyanzo vya Maji

Posted on: October 13th, 2021

NAIBU Waziri wa Maji Maryprica Mahundi amepiga marufuku kufanya shughuri za  kilimo katika maeneo ya vyanzo vya Maji.

Hayo amesema jana alipotembelea vyanzo vya Maji  katika Kata ya Mateteleka  Halmashauri ya Madaba Wilaya ya Songea Mkoa wa Ruvuma  na kukuta wananchi wamefanya uhalibifu wa Misitu inayotunza Maji.

Mara baada ya kukagua vyanzo hivyo na kufuatia malalamiko ya wananchi kupata Maji machafu ametoa tamko la kutofanya shughuli yoyote katika maeneo hayo ambayo yamesababisha  vyanzo vingine kukauka.

Mahundi amesema kuwa Maji hayana mbadala kama wananchi watatumia vibaya misitu na kulima maeneo ya vyanzo , ni lengo la Wizara ya Maji kuhakikisha kila mwanchi anapata maji umbari  mdogo ili aweze kufanya shughuli zake za kila siku kiurahisi.

“Nimekuja kuwakumbusha wanamateteleka tutunze vyanzo vya Maji,maana Maji hayana Mbadala,utapata mbadala wa kulima lakini siyo Maji”.

Naibu Waziri amesema amesikitishwa na ukataji wa miti ya  asili ambayo ilikuwa inasidia kwa kiasi kikubwa kutunza vyanzo vya Maji na kutoa tamko kuacha mara moja kufanya shughuli yoyote katika maeneo hayo.

Hata hivyo Mahundi amesema Wizara ya Maji ipo mbioni kuleta Maji katika Kituo cha afya Mateteleka ambacho Rais Samia ameleta milioni 200 kwaajili ya kuanza ujenzi wa Kituo hicho.

Mbunge wa jimbo la Madaba Joseph Mhagama amewaomba wataalamu wa RUWASA  kuwaongezea chanzo cha maji kufuatia kata Mbili kutumia chanzo kimoja imepelekea Maji kutojitosheleza kwa wananchi hao.

Imeandaliwa na Aneth Ndonde

Kutoka Ofisi ya Habari ya Mkuu wa Mkoa Ruvuma

Octoba 13,2021.

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Chwaya atoa rai kwa walimu wa awali kutekeleza agizo la Serikali

    January 18, 2025
  • MARATIBU wa mradi wa BOOST Madaba amshukuru Rais Samia

    January 18, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa