• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

MKUU wa Mkoa wa Ruvuma amewaagiza Viongozi kusimamia utunzaji vyanzo vya Maji

Posted on: February 1st, 2021

MKUU wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme amewapongeza wadau wa sekta ya Maji Ruvuma kwa utekelezaji wa miradi ya  Maji vijijini na Mijini.

Hayo amesema alipokuwa akifungua kikao cha wadau wa sekta ya maji katika ukumbi wa Manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma na kuwapa heko wananchi wanaojenga miradi hiyo kwa kujitegemea.

“Ili tuweze kufanya tathimini ya utendaji kazi na uwajibikaji katika usimamizi na utekelezaji  wa miradi ya maji na kuhakikisha inakuwa endelevu lazima Halmashauri na sekretalieti ya Mkoa muwajibike kikamilifu katika kutekeleza,  kusimamia majukumu yote yaliyoorodheshwa kwenye sheria na 5 ya huduma ya maji mwaka 2019”.

Mndeme amesema Meneja wa RUWASA  kwa kushirikiana na Halmashauri zihakikishe miradi hiyo na mingine inajengwa na kuunda vyombo huru vya watumia maji na 5 ya mwaka 2019 ifikapo Mei 31, 2021.

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma amewaagiaza  Maafisa Tarafa,Viongozi wote ngazi ya Wilaya  na Wakuu wa Wilaya kusimamia utunzaji wa vyanzo vya Maji.

Hata hivyo amesema kikao cha Baraza la Madiwani cha kila robo mwaka iwepo mada ya  kudumu ambapo Meneja RUWASA(W) watoe taarifa kuhusu uundaji na usajili wa vyombo vya watumia maji.

Mndeme ameendelea kuwaagiza Mameneja wa RUWASA wa Wilaya kufanya kazi kwa kushirikiana na ofisi za serikali zilizopo kwenye wilaya zao, Halmashauri za serikali za mitaa zote,Ofisi ya Ruwasa Mkoa wa Ruvuma, na Mamlaka ya maji safi  wa Mazingira SOUWASA zikishirikiana na ofisi ya Mabonde ya Maji katika kutafuta vyanzo vya maji  na kuandaa  mpango wa utunzaji wa vyanzo hivyo.

Pia amesema Ofisi za RUWASA Mkoa wa Ruvuma na Mamlaka ya Maji safi  na Usafi wa Mazingira SOUWASA zitumie maabara  zilizo kwenye ofisi  za mabonde ya maji ili kubainisha ubora wa maji  katika kubainisha vyanzo vya maji  kwaajili ya miradi.

Amesema Fedha na mauzo ya maji zikaguliwe na wakaguzi wa ndani wa Halmashauri ili kujiridhisha na matumizi ya fedha za wananchi na kuendelea kuchua hatua stahiki kwa wananchi wanao haribu kwa maksudi miundombinu ya maji na vyanzo vya maji.

Imeandaliwa na Aneth Ndonde

Afisa Habari Halmashauri ya Madaba

Februari 1,2021.

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Chwaya atoa rai kwa walimu wa awali kutekeleza agizo la Serikali

    January 18, 2025
  • MARATIBU wa mradi wa BOOST Madaba amshukuru Rais Samia

    January 18, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa