• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

MKUTANO MKUU WA 32 WA WINO SACCOS WAFANA MADABA

Posted on: October 25th, 2025

Mkutano Mkuu wa 32 wa Wajumbe Wawakilishi wa WINO SACCOS umefanyika katika Ukumbi wa WIDA, kijiji cha Lilondo, Wilaya ya Madaba, ambapo umehudhuriwa na viongozi, watendaji na wanachama wa chama hicho cha ushirika.

Akizungumza katika mkutano huo, Afisa Ushirika wa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba, Ndugu Sadam Fupi, amewataka viongozi na watendaji wa WINO SACCOS kuendelea kusimamia misingi ya ushirika kwa kuhakikisha huduma bora zinatolewa kwa wanachama na jamii kwa ujumla.

Aidha, Ndugu Fupi amesisitiza umuhimu wa kufuatilia mikopo iliyocheleweshwa kurejeshwa, akibainisha kuwa ucheleweshaji wa marejesho unaathiri maendeleo ya chama na kuleta taswira ya kutowajibika kwa baadhi ya wanachama.

Katika mkutano huo, ilielezwa kuwa Wino SACCOS imepata hati safi kutoka kwa Mkaguzi wa Vyama vya Ushirika, jambo lililopongezwa na wajumbe wote kama ishara ya uwajibikaji na utunzaji mzuri wa mali za chama. Aidha, imeelezwa kuwa jumla ya wanachama 212 wamefikisha hisa zao.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi ya WINO SACCOS, aliwashukuru wajumbe na watendaji wote kwa ushirikiano wao, huku akisisitiza umuhimu wa kuyatekeleza maazimio yote yaliyopitishwa katika mkutano huo kwa pamoja.

Naye mwakilishi kutoka Chuo cha Ushirika Moshi, Ndugu Benitho, aliwataka wanachama kuongeza hisa zao ili kuboresha mtaji wa chama na kujihakikishia uanachama halali. Pia aliwakumbusha kutunza nyaraka zote muhimu za taasisi na aliupongeza mkutano kwa kuwa wa “kisayansi” unaolenga utekelezaji wa maazimio kwa vitendo.



Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • WAHITIMU WA UFUNDI STADI KUPATIWA VIFAA VYA KUANZIA KAZI VYENYE THAMANI YA MILIONI 4.4

    November 27, 2025
  • WATAALAMU WA AFYA NGAZI YA MSINGI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MADABA WAANZA MAFUNZO MAALUM YA KUBORESHA HUDUMA KWA WAZEE

    November 26, 2025
  • DC NDILE ATOA MAELEKEZO YA KUIMARISHA AFUA ZA LISHE MADABA

    November 25, 2025
  • UHISHWAJI WA BARAZA LA WAZEE MADABA WAFANYIKA LITUTA.

    November 22, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa