• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

MKUTANO MKUU WA 28 WA CHAMA CHA USHIRIKA WA AKIBA NA MIKOPO MAHANJE WAFANA MADABA

Posted on: October 18th, 2025

MADABA, 18 OKTOBA 2025 – Mkutano Mkuu wa 28 wa Chama cha Ushirika wa Akiba na Mikopo Mahanje (MAHANJE SACCOS) umefanyika leo katika Ukumbi wa Amani, ukiwaleta pamoja wanachama, viongozi na wadau wa ushirika kwa lengo la kujadili maendeleo na mikakati ya kuimarisha huduma za kifedha ndani ya chama.

Mkutano huo ulifunguliwa rasmi na Afisa Ushirika wa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba, Ndugu Sadam Fupi ambaye alitoa wito kwa wanachama kuendelea kuimarisha ushirika kwa kuweka akiba, kukopa na kununua hisa, ili kukuza mtaji wa chama na kuhakikisha uendelevu wake.

Ndugu Fupi alisema kuwa, maendeleo yanayoonekana ndani ya MAHANJE SACCOS ni ishara kwamba wanachama na viongozi wanafanya kazi kwa bidii na uwajibikaji, akisisitiza kuwa ushirika ni chombo muhimu katika kuinua kipato cha wananchi wa kipato cha chini.

Aidha, aliwataka viongozi wa chama hicho kusimamia shughuli za SACCOS kwa kufuata sheria, kanuni na taratibu za ushirika, huku akihimiza uadilifu na uwazi katika matumizi ya fedha.

Katika mwaka wa 2025, MAHANJE SACCOS imepata mafanikio makubwa ikiwemo Kutoa mikopo kwa wanachama yenye thamani ya TZS Milioni 319.3, Kushinda Tuzo ya SACCOS Bora Tanzania kwa kundi la uwezeshaji wa vijana katika sekta ya kifedha, iliyotolewa na Tume ya Maendeleo ya Ushirika Tanzania (TCDC), Kushika nafasi ya pili kitaifa kwa SACCOS bora za kijamii Daraja A, Ukaguzi wa hesabu kufikia mwaka 2024 na COASCO, ulioonesha usimamizi mzuri wa fedha pamoja na Ongezeko kubwa la wanachama katika kipindi cha Januari hadi Septemba 2025.

Katika mkutano huo, wanachama walipata fursa ya kupitia taarifa mbalimbali na mapendekezo ya kuboresha huduma za mikopo na uwekaji wa akiba. Pia, baadhi ya wanachama walipewa pongezi na kupatiwa vyeti kwa mchango wao mkubwa katika kukuza hisa na kuhamasisha wengine kushiriki kikamilifu.

Mkutano huo uliendelea kwa mijadala ya ajenda kuu za chama, ikiwemo tathmini ya utendaji wa mwaka uliopita na kupanga mikakati mipya ya kuboresha huduma kwa wanachama, kabla ya kufungwa rasmi na Kamati Kuu ya SACCOS.

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • UHISHWAJI WA BARAZA LA WAZEE MADABA WAFANYIKA LITUTA.

    November 22, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MADABA YAPEWA CHETI CHA PONGEZI KWA UTEKELEZAJI BORA WA LISHE

    November 21, 2025
  • TIMU YA UKAGUZI MKOA WA RUVUMA YAFURAHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MADABA.

    November 08, 2025
  • TIMU YA UKAGUZI KUTOKA MKOANI YATUA MADABA KWA UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO.

    November 06, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa