• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

MKOA wa Ruvuma ulivyoshika nafasi ya kwanza kitaifa ukusanyaji wa mapato

Posted on: April 16th, 2021

Mkoa wa Ruvuma  mwezi Machi mwaka huu umeshika nafasi ya kwanza kitaifa katika ukusanyaji wa mapato kupitia TRA  baada ya kukusanya kwa asilimia 159.

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme akizungumza na watendaji wa serikali na Taasisi za umma kutoka wilaya zote tano mkoani hapa,amesema hivi sasa Mkoa wa Ruvuma upo katika mikoa kumi bora inayochangia Pato la Taifa.

“Huwezi kuamini,mwezi Machi mwaka huu,Mkoa wa Ruvuma tumekuwa wa kwanza kitaifa katika ukusanyaji mapato kupitia TRA,tukusanya kwa asilimia 159,haya ni makusanyo ya serikali kuu inahusika mikoa yote nchini’’,alisema Mndeme.

Hata hivyo amesema Mkoa wa Ruvuma umekuwa kinara katika ukusanyaji wa mapato,ambapo kuanzia Julai hadi Desemba 2020,Mkoa wa Ruvuma umekuwa Mkoa wa pili kitaifa katika ukusanyaji wa mapato kupitia TRA na serikali imetoa tuzo kwa Mkoa.

Amempongeza Meneja wa TRA Mkoa wa Ruvuma pamoja wafanyakazi wote kwa ujumla kwa kusimamia ipasavyo ukusanyaji mapato kwa kiwango kilicholeta tija licha ya kukabiliwa na changamoto mbalimbali katika ukusanyaji wa mapato.

“Kazi ya kukusanya mapato ni ngumu,ina changamoto nyingi kwa sababu hakuna mtu anayependa kulipa kodi,ukusanyaji mapato ni muhimu kwa maendeleo kwa sababu serikali inatumia fedha zilizokusanywa kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo barabara,umeme,elimu na miradi mingine ya kimkakati.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Aprili 16,2021

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Chwaya atoa rai kwa walimu wa awali kutekeleza agizo la Serikali

    January 18, 2025
  • MARATIBU wa mradi wa BOOST Madaba amshukuru Rais Samia

    January 18, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa