• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

MIKAKATI 5 ya ufundishaji aliyotoa Kairuki

Posted on: January 11th, 2023

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais Tamisemi Angela Kairuki ametoa amaagizo kuhakikisha Walimu wanakuwa na mikakati ya  kuboreha ufundishaji  kwa wanafunzi  Mkoani Ruvuma.

Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo Dkt Julias Ningu amemwakilisha Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tamisemi Angela Kairuki katika kikao Kazi kilichofanyika katika ukumbi wa Shule ya Songea girls Manispaa ya Songea na kujumuisha Wakurugenzi wa Halmashauri zote nane,Maafisa Elimu,na walimu wa Kuu wa Shule zote.

Akizungumza katika kikao kazi hicho Ningu amesema kwa niaba ya Waziri wa Nchi ofisi ya Rais Tamisemiamewataka kuandaa  mikakati ya ufundishaji  na namna ya kumfanya mwanafunzi aelewe na itasaidia kuleta tija katika Sekta ya Elimu na kuondoa changamoto ya kusababisha dondoko  katika Mkoa wa Ruvuma na Nchi nzima .

Amesema kila Afisa Elimu afanye ufuatiliaji mashuleni  angalau shule 2 kila siku  na kushauriana na walimu kikamilifu juu ya ufundishaji  baada ya kukaa ofisini.

Walimu wajiwekee malengo binafsi katika masomo wanayofundisha pamoja na kutambuliwa kwa  kazi yao kuhakikisha wanatiwa moyo na kuto  dhalilishwi na mtu yoyote.

“ kila kiongozi ahakikishe wanafunzi  wa Shule za msingi na Sekondari wanakula Shuleni pamoja na kuhakikisha  anaimalisha uwajibikaji  wa watumishi wote katika ngazi zote ili kuongeza tija katika utendaji kazi”.

Hata hivyo amesema Walimu wanabahati kubwa sana kwa sababu ni wito ni cheo ambacho hakina kustaafu lakini baada ya kustaafu bado wanaendelea kuitwa walimu inaweza kuwa sababu ya msingi Mwalimu Nyerere katika majina yake alipenda kuitwa  Mwalimu.

Naye Naibu Mkurugenzi Tamisemi Suzan Nusu akimwakilisha Naibu katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tume ya Utumishi wa Elimu Mwl. Pauline Nkwama amesema Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Kassim Majaliwa alizindua rasmi miongozo ya usimamizi na utekelezaji wa mikakati ya kuboresha Elimu nchini Agosti 4,2022”.

“Kupitia miongozo ile iligawika Miokoa yote ,Mkoa wa  Ruvuma mlifanya vizuri nakili kuhakikisha kuanzia ngazi ya Mkoa Halmashauri mpaka kata”.

Amesema kupitia mikakati hiyo Waziri wa Tamisemi ameelelekeza kukutana na wadau wa Elimu kuelekezana kupewa maagizo kila mtu asimame kwa nafasi yake kuhakikisha jambo watakalokubalina leo lipitishwa na litekelezwa.

Hata hivyo amesema kupitia kikao hiki ngazi ya Wizara wapo kwaajili ya kuweka mikakati na mitazamo ya Serikali  pamoja na usimamizi na uendelezaji wa Elimu mwaka 2023  ifikapo Januari 2024 wawe na Lugha moja bila kumtisha mtu bali kufukia malengo ya Wizara ya Rais Tamisemi.

“Mheshimiwa Rais amewekeza sana katika Sekta ya Elimu tufike mahali tuone jitihada za Rais tumekuwa tukifanya vizuri lakini yapo maeneo machache yanatukwamisha hivyo  kwa lugha nyingine ya Kikristo kupitia kikao hiki tumebatizwa upya”.

Imeandaliwa na Aneth Ndonde

Kutoka Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Madaba

Januari 11,2023.

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • WAHITIMU WA UFUNDI STADI KUPATIWA VIFAA VYA KUANZIA KAZI VYENYE THAMANI YA MILIONI 4.4

    November 27, 2025
  • WATAALAMU WA AFYA NGAZI YA MSINGI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MADABA WAANZA MAFUNZO MAALUM YA KUBORESHA HUDUMA KWA WAZEE

    November 26, 2025
  • DC NDILE ATOA MAELEKEZO YA KUIMARISHA AFUA ZA LISHE MADABA

    November 25, 2025
  • UHISHWAJI WA BARAZA LA WAZEE MADABA WAFANYIKA LITUTA.

    November 22, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa