• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

Mfahamu Twiga anayepatikana katika hifadhi za wanyamapori Tanzania

Posted on: December 28th, 2020

TANZANIA ni nchi ambayo inahifadhi nyingi za wanyamapori, Mkoa wa Ruvuma ni Miongoni mwa hifadhi za  Wanyama pori wenye sifa ya kujamiiana kwaajili ya uzazi tu.

Akizungumzia Mnyama aina ya Twiga afisa maliasili  Msaidizi kituo cha  Taarifa za Utalii Mkoa wa Ruvuma ABdallah Omary Ambani amesema ni mnyama anayejamiiana kwa sekunde 3 na kupumzika kwa masaa 2 na kurudia tena sekunde 3 na kubeba mimba miezi kumi na nne mpaka kumi na tano na kuzaa mtoto 1

Amesema mnyama huyo anajamiana kwa mda mfupi kwa sababu anashinikizo la damu na akijamiiana kwa mda mrefu anaweza kuhatarisha maisha  yake na analala kwa dakika ishirini, kutokana na tabia hiyo kumpelekea kuishi kwa mda wa miaka 25 mpaka 40.

“Twiga anazaa mtoto ambae anajiweza baada ya kuzaliwa anakaa dakika kumi na tano mpaka ishirini kuanza kutembea kutokana na mazingira anayoishi anamaadui wengi sana,inaweza kupekea kupungua kwa wanyama hao”.

Amesema wanyama hao katika Mkoa wa Ruvuma wanapatikana katika hifadhi ya Liparamba,Gesi Masoa,Hifadhi ya Nyerere na Litumbandyosi

Ambani amesema mnyama huyo licha ya sifa hiyo anasifa nyingi nyingi katika maisha yake ikiwemo kuwa na viungo virefu na kuwa na pembe zenye nywele na zinamsaidia kuchukua hewa angani na kupeleka kwenye mishipa yake ya damu pia kupambana na maadui.

Amesema Twiga anaupekee wa  kuishi katika miti ya Migunga na miti hiyo inamiba mingi kupitia mdomo wake uliochongoka na pua yake imeziba inamsaidia kula majani ya mti huo bila kupata madhara yoyote.

Hata hivyo ameendelea kumwelezea mnyama huyo kuwa ana Ulimi mrefu na Mgumu unamwezesha kutopata madhara anapokula majani kwenye miti hata kwenye macho yake yana  nundu zinamsaidia kutochomwa na miiba hiyo anapokuwa anakula.

Afisa maliasili msaidizi amesema mnyama huyo kutokana na urefu wake hupendelea kula miti mirefu na majani ya katikati na inampelekea kutokunywa maji mara nyingi kutokana na chakula anachokula ikiwa wanyama wengine kunywa maji zaidi ya mara 5 kwa siku.

“Mnyama huyo miguu yake ni mirefu inamsaidia kupambana na maadaui anapiga mateke mbele na nyuma anaweza kumuua hata Simba pia ni mnyama mpole lakini akichokozwa anakuwa mkali,na mkia wake ni mrefu humsaidia kufukuza wadudu wanaotua katika mwili wake”.

Akielezea kuwa mnyama huyo anapoenda kunywa maji wanakuwa kundi lakini wanakunywa kwa kusubiliana ili kujilinda dhidi ya maadui na wanapenda kujichanganya na wanyama waaina nyingine wanapokuwa katika matembezi ili kujua kama kuna maadui.

Imeandaliwa na Aneth Ndonde

Afisa Habari Halmashauri ya Madaba

Desemba  28,2020.

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • UJENZI WA MADARASA 2 NA MATUNDU 6 YA VYOO SHULE YA MSINGI KIPINGO WAKAMILIKA KWA ASILIMIA 100

    May 30, 2025
  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Chwaya atoa rai kwa walimu wa awali kutekeleza agizo la Serikali

    January 18, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa