MBUNGE wa Jimbo la Madaba Joseph Mhagama amewashukuru Viongozi wa wa Kata ya Wino na Wananchi kwa Kumsaidia kutekeleza majukumu yake.
Hayo amezungumza katika hafla iliyoandaliwa na viongozi wa Kata ya Wino ya kumpongeza Mbunge huyo kwa utekelezaji wa miradi mbalimbali ya Maendeleo aliyoleta katika Kata hiyo.
“Nashukuru sana kwa kunibeba Waheshimiwa Madiwani mmesimama na mimi Mbunge kutekeleza majukumu yangu ambayo niliwaahidi wananchi asanteni sana kupitia hayo yote najiona ninadeni na ninyi.”.
Mhagama amesema wananchi wa Kata ya Wino wamefungua safari mpya ya uongozi wake kwa kufanya kuwa siku ya historia kama mbunge wa Jimbo la Madaba hivyo ameahidi kuendelea kuleta maendeleo mbalimbali katika Jimbo hilo.
“Siku ya leo mmeitenga kumshukuru Mungu kwa neema na Baraka ambazo sisi wanamadaba tumepata kupitia mimi Mbunge na mwakilishi wenu nitaendelea kuleta maendeleo Madaba’’
Aidha amesema maendeleo hayataletwa na mtu mmoja bali kila mtu kwa nafasi yake ili kuhakikisha ushirikiano na umoja unaleta matokeo yanayoonekana kwa maombi,kwa kutoa Baraka,kwa kumsemea kiongozi vizuri.
Kutoka Kitengo cha Mawasiliano Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
Julai 9,2024
MADABA - RUVUMA
Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA
Simu: 0252951052
Simu ya Mkononi:
Barua pepe: ded@madabadc.go.tz
Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa