• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

MBIO za Mwenge wa Uhuru Ruvuma kuanza Aprili 17 na kukabidhi Mkoa wa Njombe Aprili 25

Posted on: February 25th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanal. Laban Thomas amewataka viongozi na Wataalamu Mkoani Ruvuma kuhakiksha wanafanya ukaguzi wa  nyaraka za miradi yote itakayotembelewa na mwenge ili kujiridhisha na hatua ya  utekelezaji wa mradi husika.

Amesema kila kiongozi katika nafasi yake anapaswa kuwajibika katika kutekeleza   majukumu yake ya kazi ikiwemo   na kujenga ushirikiano katika kusimamia  miradi yote inayotekelezwa ngazi ya Halmshauri na kufikia lengo lililokusudiwa.

Hayo yamejili  katika kikao cha maandalizi ya mapokezi ya Mwenge wa Uhuru mwaka 2023 Mkoani Ruvuma kilichofanyika leo tarehe 24 Februari katika ukumbi wa Manispaa ya Songea ambapo kilihudhuriwa na viongozi ngazi ya Mkoa, Wakuu wa Wilaya, Mkatibu tawala Wilaya, Wakurugenzi wote, Waratibu wa Mwenge kila Halmashauri, pamoja na kamati ya ulinzi na usalama, kilichofanyika kwa lengo la  kupokea tathimini ya Mbio za mwenge wa Uhuru 2022 na maandalizi ya mapokezi ya Mwenge wa Uhuru 2023.

Kanal. Laban amesema Mbio za Mwenge wa Uhuru kwa mwaka 2023 Mkoani Ruvuma zitaanza rasmi tarehe 17 Aprili 2023, ambao Mwenge utapokelewa ukitokea Mkoa  wa Lindi na mapokezi yatafanyika katika kijiji cha Sauti  Moja,  Wilayani  Tunduru  ambapo utakimbizwa katika Halmashauri 8 nane na kukabidhiwa katika Mkoa wa Njombe  kijiji cha Kipingu tarehe 25 Aprili 2023.”Alibanisha”

Kwa mwaka 2022 Mkoa wa Ruvuma ulipokea Mwenge wa Uhuru  tarehe 08 April 2022 katika kijiji cha Lituhi Wilaya ya Nyasa na ulikabidhiwa kwa uongozi wa Mkoa wa Mtwara  tarehe 16 April  2022 katika kijiji cha Lumesule Wilaya ya Nanyumbu.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Ruvuma Oddo Mwisho amesema Chama cha Mapinduzi kina wajibu wa  kutembelea miradi na kufanya  ukaguzi wa   miradi yote inayotekelezwa na Serikali ili  kujiridhisha  kila  hatua ya mradi  katika  Halmashauri.

Komredi Oddo amewataka wataalamu wte Mkoani Ruvuma kuhakikisha wanaweka kumbukumbu za kila mradi ambao utatembelewa na Mwenge ili kujirisha na utekelezaji wake.

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MADABA YAPONGEZWA KWA KUPATA HATI SAFI KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    June 19, 2025
  • UJENZI WA MADARASA 2 NA MATUNDU 6 YA VYOO SHULE YA MSINGI KIPINGO WAKAMILIKA KWA ASILIMIA 100

    May 30, 2025
  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa