• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

MAKARANI MADABA WAAPISHWA, Waaswa Kudumisha Uadilifu Kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025.

Posted on: October 25th, 2025

Msimamizi Mkuu wa Uchaguzi wa Jimbo la Madaba, Wakili Abdul M. Manga, ameongoza mafunzo maalum kwa Makarani Waongozaji wa Vituo vya Kupigia Kura yatakayohusika katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025. Mafunzo hayo yamefanyika katika ukumbi wa Shule ya Sekondari Madaba Day, yakilenga kuongeza uelewa na uadilifu wa watendaji hao kuelekea uchaguzi huo muhimu wa kitaifa.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo, Wakili Manga amewataka Makarani hao kufanya kazi kwa uwazi, uadilifu na kutokuegemea upande wowote wa kisiasa, huku wakizingatia misingi ya demokrasia na katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

 “Ni vyema mkatambua kwamba, kwa mujibu wa Ibara ya 74(6) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) ndiyo yenye mamlaka ya kusimamia na kuratibu uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani,” alisema Ndg. Manga, akisisitiza wajibu wa kikatiba wa watendaji hao katika kuhakikisha uchaguzi unakuwa huru na wa haki.

Mafunzo hayo pia yaliambatana na viapo vya kutunza Siri na kujitoa uanachama, lakini pia kua na uaminifu na uadilifu, vilivyoapishwa kwa Makarani wote waongozaji wa vituo vya kupigia kura, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya kuhakikisha zoezi la upigaji kura linaendeshwa kwa weledi.

Jumla ya Makarani kutoka vituo 132 vya kupigia kura vilivyopo katika kata nane za Halmashauri ya Wilaya ya Madaba walihudhuria mafunzo hayo.

Washiriki walipata nafasi ya kuuliza maswali, kutoa maoni na kujadiliana kuhusu mbinu bora za kusimamia uchaguzi. Waliahidi kutekeleza viapo vyao kwa uaminifu ili kuhakikisha wananchi wanapata haki yao ya kikatiba ya kuchagua viongozi wanaowataka kwa amani na utulivu.

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • UHISHWAJI WA BARAZA LA WAZEE MADABA WAFANYIKA LITUTA.

    November 22, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MADABA YAPEWA CHETI CHA PONGEZI KWA UTEKELEZAJI BORA WA LISHE

    November 21, 2025
  • TIMU YA UKAGUZI MKOA WA RUVUMA YAFURAHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MADABA.

    November 08, 2025
  • TIMU YA UKAGUZI KUTOKA MKOANI YATUA MADABA KWA UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO.

    November 06, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa