• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

MAFUNZO YA WASIMAMIZI WA VITUO NA WASIMAMIZI WASAIDI YAFUNGWA RASMI, MSISITIZO WAWEKWA KWENYE UZALENDO NA UADILIFU.

Posted on: October 27th, 2025

Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Madaba, Wakili Abdul Manga, amefunga rasmi mafunzo ya siku mbili kwa Wasimamizi wa Vituo na Wasimamizi Wasaidizi wa Vituo vya Kupigia Kura yaliyofanyika katika ukumbi wa Shule ya Sekondari Madaba.

Akizungumza wakati wa hafla ya kufunga mafunzo hayo, Wakili Manga aliwataka wasimamizi wote kufanya kazi zao kwa uzalendo, uadilifu, ushirikiano na weledi wa hali ya juu, akisisitiza kuwa jukumu walilopewa ni la kizalendo na linahitaji nidhamu na uwajibikaji mkubwa.

“Kazi mnayoenda kufanya ni ya kizalendo na ya kulinda demokrasia ya nchi yetu. Fanyeni kazi kwa weledi, kwa kuzingatia maelekezo, na msikubali kufanya makosa ya uzembe ambayo yanaweza kuharibu mchakato wa uchaguzi,” alisema Wakili Manga.

Miongoni mwa mambo yaliyosisitizwa katika mafunzo hayo ni pamoja na:

Kufanya kazi kwa uzalendo na weledi, wakitambua kuwa uchaguzi ni wa taifa zima.

Kufuata maelekezo ya Msimamizi wa Kituo kama kiongozi mkuu wa kituo husika.

Kuhakiki vifaa vya uchaguzi kwa haraka mara baada ya kuvipokea, na kutoa taarifa mapema iwapo kutakuwa na upungufu.

Kujenga ushirikiano wa timu na kuhakikisha hakuna anayeondoka kituoni bila maelekezo ya msimamizi mkuu.

Kutumia lugha nzuri kwa wapiga kura na kuwapa kipaumbele watu wenye mahitaji maalum.

Aidha, Wakili Manga aliwakumbusha maafisa hao kuwa wamebakisha siku chache kabla ya siku ya uchaguzi, hivyo ni muhimu kutumia muda uliosalia kujisomea kwa kina kitabu cha maelekezo ya wasimamizi ili kuongeza uelewa na kujiamini.

Mafunzo hayo ni sehemu ya maandalizi ya uchaguzi mkuu unatarajiwa kufanyika tarehe 29 Oktoba, 2025, ambapo wananchi wanatarajia kuchagua Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mbunge na Diwani.




Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • UHISHWAJI WA BARAZA LA WAZEE MADABA WAFANYIKA LITUTA.

    November 22, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MADABA YAPEWA CHETI CHA PONGEZI KWA UTEKELEZAJI BORA WA LISHE

    November 21, 2025
  • TIMU YA UKAGUZI MKOA WA RUVUMA YAFURAHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MADABA.

    November 08, 2025
  • TIMU YA UKAGUZI KUTOKA MKOANI YATUA MADABA KWA UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO.

    November 06, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa