• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

MADABA waishukuru Serikali kwa kuwapatia Maji Safi na Salama

Posted on: October 29th, 2021

WANANCHI wa kijiji cha Igawisenga Halmashauri ya Madaba mkoani Ruvuma,wameishukuru Serikali ya awamu ya sita kwa kuanza kutekeleza mradi mkubwa wa maji unaokwenda kumaliza kero ya maji safi na salama katika kijiji hicho.

Akiongea kwa niaba  ya wananchi mbele ya Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge,Mwenyekiti wa Serikali ya kijiji hicho Paul Ndikweje alisema, kwa muda mrefu  hawajawahi kupata maji ya bomba na hivyo kulazimika kutumia maji ya visima vya asili.

Alisema,kujengwa kwa mradi huo ni  faraja kubwa kwao  na unakwenda kuleta matumaini mapya kwa sababu walishakata tamaa  kupata maji ya bomba hasa ikizingatiwa umbali wa kijiji hicho kutoka makao  makuu ya wilaya na mkoa.

Aidha,ameomba Wakala wa maji vijijini Ruwasa wilaya ya Songea  kuwaunganishia maji kwenye nyumba zao kwani kufanya hivyo itakuwa rahisi kuchangia gharama na kuepusha migogoro, badala ya kujenga vituo vingi vya kuchotea maji(DP).

Alisema, wako tayari kulipia gharama za kuunganishiwa maji kwenye nyumba ambapo baadhi ya wananchi wameshajiandaa kuweka fedha kidogo kidogo na wanachosubiri ni kukamilika kwa mradi huo ambao wanaamini utaharakisha maendeleo.

Meneja wa Ruwasa wilaya ya Songea Mathias Charles  alisema, mradi wa maji Igawisenga unatekelezwa kwa kutumia fedha za program ya malipo kwa matokeo na umesanifiwa kuhudumia wananchi 2,275 ifikapo mwaka 2041 ambao kwa sasa wanakadiriwa kuwa 1,336.

Alisema, gharama za  utekelezaji wa mradi huo ni Sh.216,831,229.00 ambao unatekelezwa na Ruwasa kwa kutumia wataalam wa ndani na ulianza Mwezi Februari 2021 na umefikia asilimia 80.

Kwa  pande wake Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge, ameipongeza Ruwasa kwa kutekeleza mradi huo wa maji ambao utakapo kamilika utamaliza kero ya muda mrefu ya maji  safi na salama kwa wananchi wa kijiji cha Igawisenga.

Brigedia Jenerali Ibuge, ameagiza mradi huo ukamilike kama ulivyopangwa na kuitaka Ruwasa kushirikiana na Serikali ya kijiji na wananchi namna ya kuendesha mradi huo na kutunza vyanzo  kwani hatua hiyo itasaidia wananchi kuona mradi huo ni wao na kuulinda.

Alisema, maji ni muhimu sana kwa maisha ya Binadamu na maendeleo ya Nchi yetu,hata hivyo  hajaridhishwa kuona baadhi ya vyanzo vya maji havijalindwa kikamilifu na hivyo kuleta mashaka makubwa.

Alisema, Rais Samiha Suluhu Hassan amekusudia kwa dhati kumtua ndoo mama kichwani, ndiyo maana anaendelea kutoa fedha za kujenga miradi ya maji, hata hivyo  ni lazima wananchi  waelimishwe kuhusu madhara ya kulima na kufanya shughuli mbalimbali kwenye vyanzo na hifadhi za maji.

Brigedia Jenerali Ibuge ameitaka Ruwasa na uongozi wa Bonde la Ziwa nyasa ,kuhakikisha wanatumia rasilimali na nguvu kubwa kulinda vyanzo ili visiendelee kuvamiwa na wananchi na kuweka alama ambayo itazuia wananchi kuingia katika  maeneo hayo.

Ameigiza Halmashauri ya wilaya Madaba kupitia Baraza la Madiwani, kuendelea kutoa elimu kuhusu umuhimu wa kuhifadhi mazingira na kutunza vyanzo vya maji kwa faida ya sasa na baadaye.

.

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Chwaya atoa rai kwa walimu wa awali kutekeleza agizo la Serikali

    January 18, 2025
  • MARATIBU wa mradi wa BOOST Madaba amshukuru Rais Samia

    January 18, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa