• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

MAADHIMISHO ya wanawake duniani yazinduliwa rasmi Ruvuma

Posted on: March 2nd, 2021

MAADHIMISHO ya siku ya Wanawake Duniani yameziduliwa rasmi jana Wilaya ya Songea Mkoani Ruvuma katika viwanja vya Majimaji Mjini Songea.

Katibu wa wanawake Manispaa ya Songea Joyce Mwanja akisoma Risara kwa mgeni rasimi Gilda Siluimba  Mama Askofu wa kanisa la Redeemed Mjini Songea amesema  Sisi wanawake wa manispaa ya Songea tunaungana na wanawake wote Duniani hususani nchi nzima za Afrika  kuzindua siku ya wanawake Duniani leo Machi 1.

Mwanja amesema Lengo la maadhimisho haya ni kutoa fursa ya kuelimisha jamii hasa wanawake kuhusu jitihada mbalimbali zinazofanywa na Serikali,Asasi za Kiraia,Sekta binafsi na wadau wengine katika kukuza hali ya wanawake wa kitanzania.

“Kauli mbiu ya Maadhimisho hayo inasema wanawake katika uongozi chachu kufikia dunia yenye usawa,kauli mbiu hii ina ukweli usiopingika kwa kuwa kabla wanawake hatujahamasika na kushika nafasi za uongozi katika miaka ya 1990”.

Hata hivyo ameipongeza Wizara ya Maendeleo ya jamii ,Afya,Wazee,Jinsia na Watoto kwa kutuletea kauli mbiu hii inayotukumbusha kuendelea kujitambua na kutambua nafasi zetu katika kuendeleza jamii kwa namna moja au nyingine.

Amesema mwaka 2020/2021 Julai hadi Desemba Songea Manispaa kupitia mfuko wa maendeleo ya wanawake imetolewa zaidi ya shilingi miamoja  kwa vikundi 25,na zaidi ya shilingi milioni 43 imetolewa kwa vikundi 21 kwa vijana na kwa watu wenye ulemavu imetolewa zaidi ya shilingi milioni 43.

Amesema Wilaya ya Songea imeathilika na janga la UKIMWI na mikakati iliyopangwa ni pamoja na kutoa Elimu ya kupima afya kwa Hiari,kukemea mira na desturi zinazochochea maambukizi,ngoma za usiku na ulevi wa kupindukia.

Mama Askofu Gilda Siluimba wa kanisa la Rededeemed amesema katika ufunguzi wa maadhimisho hayo amewasisitiza wanawake kufanya kazi kwa bidii na kuepuka kuwa tegemezi kwa waume zao pamoja na kulea watoto katika maadili ili nchi yetu iweze kuwa na viongozi wanawake wa ngazi ya juu.

“Chachu ya kuwa na watoto wakike wanaofanya vizuri darasani inatokana na malezi ya mama,au kupata watoto wakike ambao tunatarajia wawe viongozi inatokana na mwanamke, hivyo wanawake naomba muwalee watoto katika mazingira ya kidini ili wafanye vizuri hata wakiwa shuleni na kazini na Mungu atawasaidia”.

Imeandaliwa na Aneth Ndonde

Afisa habari Halmashauri ya Madaba

Machi 2,2021.

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Chwaya atoa rai kwa walimu wa awali kutekeleza agizo la Serikali

    January 18, 2025
  • MARATIBU wa mradi wa BOOST Madaba amshukuru Rais Samia

    January 18, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa