• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

KANISA la TAG Madaba wapata Mchungaji Mpya

Posted on: November 26th, 2023

KANISA la Tanzania Assemblies of God Madaba Sehemu ya Ruvuma Kaskazini Jimbo la Ruvuma Kati wameletewa Mchungaji Mpya wa Kanisa la Mahali pamoja Obedi Mwasyika

Mchungaji huyo ameletwa kutokana na Mchungaji Kiongozi aliyekuwa anachunga Kanisa hilo Isaya Mhagama  kufariki Machi 10,2023.

Katibu wa Jimbo la Ruvuma Kati Revi Kilatu akimwakilisha Askofu wa Jimbo hilo Joachim Mhanga amemtambulisha katika Kanisa hilo ametoa rai kwa washirika  wampokee na kumkubali pamoja na kumpa ushirikiano katika kufanya kazi ya Mungu.

“Tumkubali kama alivyo, tumpe ushirikiano ili tufaidi alichonacho atakuwa Baraka kwetu,maana alijipanga kwenda kuanzisha Kanisa Viongozi wa Juu wamemuona ahudumu Madaba”.

Hata hivyo Kilatu amelipongeza Kanisa hilo kwa ushirikiano waliouonyesha kwa kumjengea Nyumba Mjane wa Mchungaji Isaya Mhagama yenye thamani ya shilingi Milioni 8,442,000/=.

Kwa Upande wake mchungaji huyo mara baada ya kutambulishwa na kukabidhiwa katika Kanisa hilo  amewaomba washirika kumpa ushirikiano katika utendaji wa kazi ya Mungu ili waweze kusonga mbele.

Naye Mwangalizi wa Sehemu ya Ruvuma Kaskazini Islael Mtafya wa Kanisa la Mahanje amesema kuwa anamfahamu Mchungaji Obedi  tangia miaka mingi na alianza kufundisha watoto Kanisani huko Mkoani  Mbeya.

 Mtafya amewaasa  washirika hao kuhakikisha wanatoa ushirikiano  kwa Mchungaji mpya bila kutengeneza makundi ambayo yatasababisha kuharibu Kanisa badala yake  kazi ya Bwana iweze Kuimarika.

“Namshukuru Mungu kwaajili ya utulivu na ushirikiano wenu mliouonyesha kuanzia Mchungaji Kiongozi alipo fariki takribani miezi 9 mmekuwa wavumilivu Sana nawapongeza”.

Mchungaji Msaidizi wa Kanisa hilo Paulo Motela aliyechunga Kanisa hilo tangia kufariki kwa Mchungaji kiongozi amewashukuru washirika  kuanzia Mchungaji Mhagama alipofariki wamempa ushirikiano wakutosha hivyo amesema  yupo tayari kufanya kazi chini ya maelezeko ya Mchunga mpya .

“Kuanzia Mchungaji kiongozi alipofariki watu hawa walinithamani sana,kunawakati nilipitia Mazingira magumu walinifariji wakiwemo wazee wa Kanisa na Mwangalizi,hivyo nipo tayari kufanya kazi ya Mungu nikifuata maelekezo yako”.

Imeandaliwa na Aneth ndonde

Kutoka Kitengo cha Mawasiliano Halmashauri ya Madaba

Novemba 26,2023.

 

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MADABA YAPONGEZWA KWA KUPATA HATI SAFI KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    June 19, 2025
  • UJENZI WA MADARASA 2 NA MATUNDU 6 YA VYOO SHULE YA MSINGI KIPINGO WAKAMILIKA KWA ASILIMIA 100

    May 30, 2025
  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa