MRATIBU wa TASAF Halmashauri ya Wilaya ya Madaba Maryam Sibuga na timu yake wamejifunza juu ya ujenzi wa soko kupitia Mradi wa TASAF katika Halmashauri ya Wilaya ya Songea.
Sibuga akizungumza kabla ya kufika eneo lililojengwa mradi huo wa soko hilo lililogharimu kiasi cha shilingi Milioni 202 pamoja na nguvu za wananchi amesema wameenda kujifunza walivyofanikiwa kutekeleza mradi na changamoto walizokutana nazo ili waweze kujua pakuanzia na mwisho wafanye vizuri zaidi.
Amesema Halmashauri ya Madaba katika ujenzi huo Serikali imetoa Milioni 171,176,339.29 kupitia mradi wa TASAF utakaosaidia kutatua changamoto za wananchi wa Halmashauri hoyo na kujipatia eneo nzuri la kufanyia Biashara zao.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea Neema Magembe amsema katika maisha na utendaji kazi kujifunza ni jambo la msingi katika Nyanja zote hata kwa Yule aliyefeli kunakuwa na chakujifunza.
Magembe amewapongeza wataalamu pamoja na Kamati ya Ujenzi wa Halmashauri ya Madaba kwenda kujifunza katika Halmashauri ya Songea amesema wamejenga soko hilo lenye vizimba 82 na matundu ya vyoo 6 na wamekutana na changamoto mbalimbali.
“Pamoja na changamoto zote adhima ya Serikali kupata Sokola wananchi, changamoto tunapokutana nazo lazima tupate ufumbuzi ili tuweze kusonga mbele”
Amesema soko hilo lilizinduliwa na mbio za Mwenge wa Uhuru Aprili 21,2023 ikiwa wananchi wamefurahia Mradi huo unaopelekea kufanya biashara katika Soko hilo.
Imeandaliwa na Aneth Ndonde
Kutoka Kitengo cha Mawasiliano Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
Agosti 29,2023.
MADABA - RUVUMA
Anwani ya Posta: P.O.BOX 10
Simu: 0252951052
Simu ya Mkononi:
Barua pepe: info@madabadc.go.tz
Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa