• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

IFINGA Madaba kunufaika na Uhifadhi

Posted on: March 11th, 2024

HALMASHAURI ya Wilaya ya Madaba Mkoa wa Ruvuma inajumla ya eneo  la hekta elfu 37,000 ya kuzalisha biashara ya hewa okaa kupitia kutunza mistu ya asili na uhifadhi wa wanyamapori.

Hayo amesema Afisa Mkuu wa wanyamapori Wizara ya Maliasili na Utalii anayesimamia uhifadhi na ushirikishwaji kwa jamii (WMA) Rose Geradi  alipozungumza na Jumuiya ya uhifadhi kijiji cha Ifinga  katika kikao cha tathimini ya kuangalia nyaraka zilizopo ili iweze kusajiliwa na kuanza kufanya kazi.

“Leo tupo kijiji cha Ifinga kuazisha hifadhi ya wanyamapori jamii tumeangalia tathimini ya awali kama wanakidhi vigezo vya uhifadhi (WMA)  ili kukamilisha zoezi la usajili kwa mujibu wa kanuni ya mwaka 2018”.

Hata hivyo  Meneja Miradi  wa shirika  lisilo la kiserikali Honeyguide linalowezesha mafunzo ya Jumuiya za Uhifadhi ukanda wa kusini mwa Tanzania Sylvester  Mselle ametoa rai kwa viongozi wa Jumuiya hiyo kuwa na uongozi bora pamoja na menejimenti na kusimamia utaratibu wa askari watakao linda maeneo.

“Bila uongozi bora hatuwezi kupata wawekezaji wala hatuwezi kujua jinsi ya kuingia mikataba lakini uongozi ukiwa thabiti mtaweza kufuata taratibu na kanuni”.

Mselle amesema shilika hilo linafanya kazi kwa ukaribu na Serikali na  linawajengea uwezo jumuiya ili waweze kuwa na uongozi na usimamizi bora ambao utapelekea kulinda rasilimali na kuweza kupata wawekezaji wengi.

 Kwa upande wake Afisa wanyamapori Halmashauri ya Madaba Ernest Nombo ameyasema matarajio katika kijiji hicho mara baada ya usajili wa jumuiya hiyo ikiwa kijiji hicho kina hekta 37000 za uhifadhi.

“Baada ya kukamilisha zoezi la usajili wa uhifadhi wananchi watafaidika watakuwa ni sehemu ya usimamizi,watapata fedha kutoka kwenye block,fedha za utalii pamoja na kuwa na askari ambao watakuwa walinzi wa eneo na kupambana na wanyama wakali”.

Kutoka Kitengo cha Mawasiliano Halmashauri ya Madaba

Machi,11,2024

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • UJENZI WA MADARASA 2 NA MATUNDU 6 YA VYOO SHULE YA MSINGI KIPINGO WAKAMILIKA KWA ASILIMIA 100

    May 30, 2025
  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Chwaya atoa rai kwa walimu wa awali kutekeleza agizo la Serikali

    January 18, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa