• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

HATA Kama kunawafugaji waliingia Songea miaka 6 iliyopita bila kibali wataondoka

Posted on: February 3rd, 2023

MKUU wa Wilaya ya Songea Wilman Ndile amepiga marufuku wafugaji holela wanaoingia katika Wilaya ya Songea bila kibali.

Hayo amesema alipoongea na wananchi wa Kata ya Mahanje Halmashauri ya Madaba  kwa mara ya kwanza mara baada ya kuapishwa na kuanza kazi rasmi.

 “Mfugaji yeyote hata kama amekaa miaka sita kabla mimi sijaingia Songea na alingia bila kibali ataondoka Serikali haishindwi”.

Ndile amesema tangia enzi za  Rais wa awamu ya kwanza Hayati Nyerere Songea ilitengwa kwaajili ya kilimo na siyo ufugaji ikiwa Wilaya ambayo inazalisha nafaka na imefanya vizuri kitaifa miaka mine mfululizo.

“Ng’ombe wakiingia na kuanza kukanyaga udongo wanaharibu rutba kwasababu udongo wa Songea ni laini na Ndiomana  ikawekwa kwaajili ya kilimo”.

Hata hivyo amesema Mfugaji yeyote lazima aingi na utaratibu na kama kijiji wameridhia na wamekaa mkutano mkuu wakamjadili na kumpa kibali ataruhusiwa ikiwa bado wananchi watahitaji nyama na maziwa.

Mtendaji wa kijiji hicho Jabiri Fussi amesoma taarifa ya kijiji hicho ikiwa na jumala ya kaya 385,jumla ya wakazi 2527.

Fussi ameipongeza Ofisi ya Mkurugenzi kwa kuchangia shilingi milioni 19 kwaajili ya ujenzi wa zahanati na Mbunge wa jimbo la Madaba milioni 10.

“Serikali chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetuunga mkono milioni 225 kwaajili ya mradi wa maji kijiji cha Mahanje”.

Diwani wa Kata ya Mahanje Mheshimiwa Stephano Mahundi amemshukuru Mkuu wa Wilaya kwa kuchagua kuongea na wananchi wa kijiji hicho kwa mara ya kwanza mara baada ya kuapishwa.

Imeandaliwa na Aneth Ndonde

Kutoka kitengo cha Mawasiliano Serikalini Halmashauri ya Madaba

Februari 3,2023

 

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MADABA YAPONGEZWA KWA KUPATA HATI SAFI KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    June 19, 2025
  • UJENZI WA MADARASA 2 NA MATUNDU 6 YA VYOO SHULE YA MSINGI KIPINGO WAKAMILIKA KWA ASILIMIA 100

    May 30, 2025
  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa