Halmashauri ya Wilaya ya Madaba imepongezwa rasmi kwa kupata hati safi katika Ukaguzi wa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa mwaka wa fedha 2023/2024, hatua inayodhihirisha uwajibikaji na usimamizi bora wa rasilimali za umma.
Pongezi hizo zimetolewa leo tarehe 19 Juni, 2025, na Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma, Bi Marry Makondo, akimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Ahmed Abbas Ahmed, wakati wa mkutano maalum wa Baraza la Madiwani uliofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.
Katika hotuba yake, Bi Makondo aliwapongeza viongozi na watendaji wa Halmashauri kwa kazi nzuri iliyopelekea kupata hati safi. Alisema:
Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba, Ndg. Sajidu Idrisa Mohamed, akiwasilisha taarifa ya CAG, alieleza kuwa mafanikio hayo yametokana na utekelezaji wa hoja na maagizo ya ukaguzi kwa ufanisi, hali inayoonyesha dhamira ya Halmashauri katika kusimamia fedha za umma kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba, Mhe. Teofanes Mlelwa, aliwashukuru madiwani na wataalamu kwa ushirikiano na juhudi zao ambazo zimeiwezesha Halmashauri kupata hati safi kwa kipindi chote cha uongozi wao.
Kupatikana kwa hati safi kwa mwaka wa fedha 2023/2024 ni ishara ya mafanikio makubwa ya kiutawala, na ni chachu kwa Halmashauri kuendelea kuimarisha misingi ya uwazi, uwajibikaji na matumizi bora ya rasilimali za umma kwa maendeleo ya wananchi wa Madaba.
MADABA - RUVUMA
Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA
Simu: 0252951052
Simu ya Mkononi:
Barua pepe: ded@madabadc.go.tz
Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa