• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

HALMASHAURI ya Madaba yashika nafasi ya Kwanza kimkoa Matokeo ya Darasa la saba 2023

Posted on: December 5th, 2023

HALMSHAURI ya Wilaya ya Madaba imeongoza kwa kushika nafasi ya Kwanza ufaulu wa Matokeo ya  Darasa la Saba  kwa asilimia 87.62 Kimkoa kati ya Halmashauri 8 Mwaka 2023.

Hayo yamesemwa katika Kikao cha tathimini ya matokeo  hayo kilicho fanyika katika Shule ya Msingi Madaba na kuhudhuriwa na Waratibu Kata,Wakuu wa Shule,Wataaluma pamoja na Idara ya Elimu ngazi ya Halmashauri.

Afisa Elimu Msingi Saada Chwaya akizungumza katika kikao hicho amewapongea Walimu kwa umoja waliounyesha katika kufundisha na kumaliza mada kwa wakati na kupelekea kuwa wakwanza katika Matokeo ya Darasa la saba  Mwaka 2023 Kimkoa.

Hata hivyo Chwaya amewashukuru Walimu kwa usimamiaji wa Miradi mbalimbali ya Maendeleo ikiwemo ya BOOST,SWASH na kukamilika kwa wakati.

“Tunaboresha Miundombinu yetu  siyo kwa Wanafunzi pepekee  hata sisi walimu tunapata mazingira mazuri ya kufundishia”.

Kwa upande wake Mratibu Kata ya Matetereka Onyango Nzali akizungumza kwa niaba ya Waratibu Kata amesema ushindi wa Mtihani wa mwaka 2023 umetokana na Wakuu wa Shule na wataaluma kuwa waadilifu na waaminifu na kusababisha kuleta matokeo halisi katika Halmashauri.

“Mtakuwa mashahidi Mtihani wa Utamilifu( Mock) Mkoa tulikuwa wa 8 katika Halmashauri za Mkoa matokeo yalikuwa yetu na yalikuwa halisi kupitia hayo wakuu wa shule na wataaluma mkaona tubadilishe histoaria”.

Naye Mwalimu Mkuu wa Shule ya Wino Talfisius Mapunda akizungumza kwa niaba ya wakuu wa Shule wa Halmashauri hiyo ameipongeza Idara ya Elimu Msingi kwa Juhudi na kuhakikisha wanaleta umoja kwa Walimu katika Halmashauri ya Madaba na kupelekea kupata matokea mazuri.

“Chamsingi tusimamie taaluma kwa pamoja na mambo mengine yatakuwa salama sisi wakuu wa shule na walimu wote”.

Kutoka Kitengo cha Mawasiliano Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

Disemba 5,2023.              

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MADABA YAPONGEZWA KWA KUPATA HATI SAFI KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    June 19, 2025
  • UJENZI WA MADARASA 2 NA MATUNDU 6 YA VYOO SHULE YA MSINGI KIPINGO WAKAMILIKA KWA ASILIMIA 100

    May 30, 2025
  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa