• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

DC Songea atoa rai ukamilishaji wa Miradi Madaba

Posted on: December 6th, 2022

HALMASHAURI ya Madaba wamefanya kikao cha Baraza la Madiwani cha robo ya mwaka kuanzia Julai 2022 hadi Septemba 2022.

Akizungumza Mkuu wa Wilaya ya Songea  Pololeth Mgema katika Baraza hilo lililofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ameagiza kuhakikisha miradi  mipya ya ujenzi wa Madarasa 10 katika Halmashauri hiyo ifikapo Desemba 10,2022 iweimekamilika.

Mgema amesema atafanya ziara ya ukaguzi kwaajili ya kuangalia ukamilifu wa Madarasa pamoja na thamani ya fedha na kiwango cha ubora wa ujenzi wa miradi hiyo.

“Sina mashaka juu ya muda tulijiwekea tarehe hiyo kwasababu tunataka tukamilishe ili tuendelee na mambo mengine na madarasa hayo kwaajili ya kidato cha kwanza mpaka kufikia Januari madarasa yatakuwa yamekamilika”.

Hata hivyo Mkuu wa Wilaya ameelekeza kuhakikisha miradi ya Mda mrefu ikiwemo Hospital ya Wilaya inayojengwa kwa zaidi ya shilingi bilioni 2 kukamilika pamoja na mradi wa nyumba tano za watumishi ifikapo mwaka mpya 2023.

Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Teofanes Mlelwa akifunga kikao hicho cha Baraza amewasisitiza Madiwani kuhakikisha  wanasimamia miradi pamoja na ukusanyaji wa Mapato katika Kata zao.

Amesema ifikapo Januari 1,2023 kufuatia tarehe hiyo kuwa siku ya kupanda miti kitaifa ametoa rai kwa Mkurugenzi kutafuta eneo la kupanda miti pamoja na maeneo mbalimbali na Watendaji kata kusimamia katika maeneo yao.

Imeandaliwa na Aneth Ndonde

Kutoka kaitengo cha Mawasiliano Serikalini Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Madaba

Desemba 6,2022.

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MADABA YAPONGEZWA KWA KUPATA HATI SAFI KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    June 19, 2025
  • UJENZI WA MADARASA 2 NA MATUNDU 6 YA VYOO SHULE YA MSINGI KIPINGO WAKAMILIKA KWA ASILIMIA 100

    May 30, 2025
  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa