• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

AFISA Maendelea Halmashauri ya Mada atoa mkakati kuhakikisha asilimia 10 kuwafikia walengwa

Posted on: June 28th, 2021

KAIMU Mkuu wa Idara ya  Maendeleo ya Jamii Anitha Makota amegawa vifaa kwa Watoto wanaoishi katika mazingira magumu katika Kata tano za  Halmashauri ya Madaba  vyenye thamani ya shilingi laki tano.

Akizungumza  ofisini kwake mara baada ya kukagua  kikundi cha watu wenye Ulemavu kata ya Mateteleka chenye watu kumi na mbili wa jinsia totauti na kutembelea wajane Kata ya Mkongotema.

Makota amesema Lengo la kuonana na Wajane hao ni kuweza kuwatambua na kuwatia moyo baada ya kupoteza wenza wao na kuwaelekeza fursa zilizopo Halmashauri ya Madaba ikiwemo mikopo ya asilimi 10 kwa wanawake.

Hata hivyo amezungumzia jinsi walivyo tekeleza siku ya Mtoto wa Afrika iliyofanyika tarehe 16 Juni 2021 katika Kata ya Lituta ilihudhuriwa na Mwenyekiti wa Halmashauri na viongozi wataka na Kijiji.

“Ndani ya hii Kata ya Lituta tuliendelea kufuatilia Walevavu na kuwagundua na tumeendelea kuwalea ni sehemu ya jukumu letu kuhakikisha kwamba ile miradi wanayoindeleza inakuwa endelevu na kila Kata tumehakikisha usalama wa watoto unaenda sawasawa kama unavyotakiwa”.

Makota akizungumzia mikakati waliyoweka katika idara hiyo amesema kuhakikisha wanaleta Umoja na Mshikamano ili kuendelea kufanya kazi kwa usahihi.

“Tunamuenzi Mh. Hayati Rais Magufuli  alihimiza umoja mshikamano upendo na kufanya kazi kwa bidii na kwa hali zote hata Rais wetu Samia anasisitiza kufanya kazi kwa bidii kwa kujitoa na kuhakikisha Taifa letu linakuwa na Maendeleo”.

Amesema mkakati wa asilimia 10 kama lilivyoelekezwa  atahakikisha linaelekezwa kwa walengwa Wanawake,walemavu,na vijana kwa kuwaibulia miradi mikubwa na yenye tija  itakayowawezesha kiuchumi.

Mkakati wa kupinga ukatili wa kijinsia amesema wameendelea kutoa elimu  katika shule mbalimbali na mitaa na mara baada ya shule kufunguliwa watatoa kampeni inayopinga Ukatili  na kuelekeza namna ya kutoa taarifa.

Mkuu wa Idara pamoja na timu yake amesema  wamejipanga kutokomeza mimba za Utotoni ikiwepo Halmashauri ya Madaba watoto wanapata Mimba wakiwa na umri mdogo kwa asilimia kubwa nao wamejipanga kutoa elimu kwa wazazi na kuhakikisha watoto hao wanatuzwa.

Amesema pia katika swala zima la kupunguza maambukizi ya Virusi vya UKIMWI  wamejipanga kuwahimiza walioathirika kuendelea kutumia dawa na kwenda kliniki, ikiwemo akinamama wajawazito kwenda hospitali na kucheki afya zao mapema.

Amesisitiza kwa wanawake kuungana na kuibua miradi yenye tija ili iweze kuwaletea maendeleo katika Halmashauri ya Madaba  ilikuhakikisha wanajifunza,wanajituma na kujitegemea.

Imeandaliwa na Aneth Ndonde

Afisa Habari Halmashauri ya Mdaba

Juni 28,2021 

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MADABA YAPONGEZWA KWA KUPATA HATI SAFI KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    June 19, 2025
  • UJENZI WA MADARASA 2 NA MATUNDU 6 YA VYOO SHULE YA MSINGI KIPINGO WAKAMILIKA KWA ASILIMIA 100

    May 30, 2025
  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa