• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

RC Ibuge atoa miezi 3 vituo vya kutolea huduma za afya vifungwe mifumo ya ukusanyaji wa mapato

Posted on: June 11th, 2021

MKUU wa Mkoa wa  Ruvuma Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge ametoa maagizo ya  mfumo wa ugavi wa Bidhaa za afya.

Hayo amesema katika kikao kazi cha viongozi wa Serikali wa Mkoa wa Ruvuma kilichofanyika jana katika ukumbi wa Manispaa ya Songea.

Ibuge amesema lengo la kikao hicho ni kukumbushana kuhusu mfumo wa utoaji wa huduma bora za afya kwa wananchi na hatimaye kuimarisha uwajibikaji wa pamoja katika uendeshaji,utoaji,ufuatiliaji na usimamizi wa huduma za afya zikiwemo dawa na vitendanishi katika Mkoa wa Ruvuma.

“Usimamizi wa huduma za afya katika maeneo yetu unaofanywa na viongozi kwa kushirikiana na wananchi unaofanywa kupitia nyenzo za vikao kwa mujibu wa miongozo iliyotolewa na Wizara ya afya,Maendeleo ya jamii,Jinsia wazee na watoto”.

“ katika kikao hiki mmepata fursa ya kuzielewa nyenzo taratibu na mifumo iliyopo ili kazi ya usimamizi,ufuatiliaji na tathimini iweze kufanywa kwa umahiri mkubwa zaidi,baadhi ya mifumo hiyo ni kamati za Hospitali,Bodi za huduma za afya za Halmashauri na kamati za afya ya msingi(PHC)”

Ibuge akitoa Maelekezo kwa Viongozi hawa amesema wahakikishe vikao vinafanyika kwa mujibu wa kalenda ya vikao vya kamati na maazimio yafanyiwe kazi na Mganga mkuu wa Mkoa kupitia katibu tawala wa Mkoa atawasilisha taarifa za utekelezaji kwa mkuu wa Mkoa kila robo mwaka.

Ifikapo Septemba Mosi 2021 vituo vyote vya kutolea huduma za afya vya umma viwe vimefungwa mfumo ya kukusanya mapato (GOTHOMIS) bila kukosa na tarehe 2 septemba niwe nimepata taarifa ya utekelezaji.

Amesema mapato na matumizi ya vyanzo katika Halmashauri yawe yanajadiliwa katika vikao vyote vya kisheria kuanzia ngazi ya kituo hadi balaza la Madiwani hususani kamati za vituo vya kutolea Huduma za Afya Bodi za huduma za Afya za Halmashauri.

Hata hivyo amesema Moja ya kigezo muhimu kitakachotumika kuangalia ufanisi wa ukusanyaji wa mapato ya Halmashauri katika Mkoa wa Ruvuma kuanzia mwaka wa fedha 2021/2022 lazikma kufikia zaidi ya asilimia 80 ya mapato ya vyanzo vya sekta ya afya (NCHF,NCHF,na user fees)

Halmashauri zihakikishe vituo vyote vya kutolea Huduma za afya Umma kama Zahanati,Vituo vya afya na Hospitali vinatumika kila mwezi kwa wakati madai (claims) na mfuko wa Taifa wa  Bima ya Afya(NHIF)

Amesema Halmashauri zihakikishe uhamasishaji mkubwa wa jamii kujiunga na mfuko wa afya ya Jamii na uboreshaji wa (iCHF)hadi sasa Mkoa umefikia kuandikisha kaya zilizo hai 11,820 sawa na asilimia 3.3 lengo ni kufikia  180,085 sawa na asilimia 50 na halmashauri ziwe na bajeti na mipango ya kweli inayoakisi mapato halisi ya sekta ya afya na hatimaye kupanua wigo wa huduma bora ya afya.

 Dr.Kanga amesema mfuko wa iCHF mkoani Ruvuma ulianza kutekelezwa mwaka 2019,ambapo kitaifa Mkoa ulishika nafasi ya mwisho ambapo hivi sasa Mkoa umepanda hadi kufikia nafasi ya 11 kitaifa na kwamba kikao kazi hicho kitaongeza ufanisi na tija.

Imeandaliwa na Aneth Ndonde

Afisa Habari Halmashauri ya Madaba

Mai 11,2021

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Chwaya atoa rai kwa walimu wa awali kutekeleza agizo la Serikali

    January 18, 2025
  • MARATIBU wa mradi wa BOOST Madaba amshukuru Rais Samia

    January 18, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa