• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

HALMASHAURI ya Madaba yatoa mkopo kwa kikundi cha Mothers group zaidi ya milioni 6 ya mapato ya ndani

Posted on: January 27th, 2023

HALMASHAURI ya Wilaya ya  Madaba imetoa mkopo wa Guta kwa kikundi cha Mothers group lenye thamani ya shilingi milioni sita na laki saba (6,700,000/=) iliyotokana na mapato ya ndani.

Akikabidhi guta hilo  kwa kikundi hicho Mwenyekiti wa Hamashauri ya Madaba Teofanes Mlelwa amewaasa wanakikundi hao suala la uaminifu wa marejesho ya mkopo waliopewa ili waweze kukopeshwa tena.

“Kikubwa tambueni fedha za Halmashauri tunazo wakopesha siyo zawadi kwasababu wengine wakikopeshwa hawarudishi wakidaiwa wanasema ni mali yao mpaka tumeanza kupelekana kwenye vyombo vya sheria”.

Hata hivyo amesema kupitia mkopo huo wahakikishe wanafikia malengo waliyokusudia maana Halmashauri ya Madaba inawajali sana wanawake,vijana na wenyeulemavu ili na wengine waweze kukopa.

Kaimu Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii Bashiru Mgwasa amesema kuwa guta ni mali ya Halmashauri ya Madaba mpaka pale watakapo maliza Mkopo wao wa shilingi milioni sita na laki saba zilizotumika kununulia.

“Sasahivi umiliki utakuwa wa pande Mbili Mothers group na upande wa Halmashauri ya Madaba mtakapomaliza tutahamisha umiliki utabaki wa kikundi chenu”.

Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Olaph Pili amemponge Mwenyekiti wa  Halmashauri na Mkurugenzi pamoja na wataalamu kwa kusimamia mapato ya ndani na kuhakikisha vikundi vinakopeshwa.

Mhasibu wa kikundi hicho kwa niaba ya wenzake Stela Mkinga amewashukuru viongo wa Halamshauri kwa kuwapatia Mkopo na ameahidi kurejesha Mkopo huo kwa uaminifu na kwa wakati.

Kikundi cha mothers group mwaka 2021 walipewa mkopo wa shilingi milioni 10 kutokana na mapato ya ndani ya Halmashauri.

Imeandaliwa na Aneth Ndonde

Kutoka Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Halmashauri ya Madaba

Januari 27,2023. 

 

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • UJENZI WA MADARASA 2 NA MATUNDU 6 YA VYOO SHULE YA MSINGI KIPINGO WAKAMILIKA KWA ASILIMIA 100

    May 30, 2025
  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Chwaya atoa rai kwa walimu wa awali kutekeleza agizo la Serikali

    January 18, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa