• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

MAENEO ya uwekezaji wa Viwanda,kilimo ,Ufugaji na Biashara

Start Date: 2020-12-01
End Date: 2022-02-01

3. MAENEO YA UWEKEZAJI YALIYOTAMBULIKA YALIYOPO KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MADABA

ENEO LA EKARI 400 KWENYE MJI WA MADABA

Eneo hili la ekari 400 lipo katika kitongoji cha Ifugwa kijiji cha Madaba kilomita 10 kutoka barabara kuu ya Songea-Njombe kwenye mji wa Madaba ukielekea wilaya ya Ludewa. Ni eneo lililotengwa kwa ajili ya uwekezaji wa viwanda vya aina mbalimbali. Mwekezaji yeyote anakaribishwa na atapewa eneo la kujenga kiwanda/shughuli yoyote atakayohitaji. Aidha Halmashauri inaendelea kupima viwanja katika vijiji vyote vinavyozunguka Mji wa Madaba ambapo tunarajia kutenga maeneo mengine ya uwekezaji. 

ENEO LA ITOMBOLOLO KIJIJI CHA MKONGOTEMA 

Eneo hili la hekta 2000 lipo katika kijiji cha Mkongotema mpakani na kijiji cha Lutukila kandokando ya barabara kuu ya Songea - Njombe. Ni eneo lililotengwa kwa ajili ya shughuli za uwekezaji hasa viwanda vya kuchakata/kuongeza thamani ya mazao kama vile mahindi, tangawizi na mazao mengine.  Eneo hili ni mali ya kijiji hivyo yeyote anayehitaji, Halmashauri na Kijiji watahakikisha Mwekezaji anapata eneo analohitaji kwa ajili ya uwekezaji ili wananchi wanufaike na fursa za kazi zitakazojitokeza.

SHAMBA LA MIFUGO HEKTA 4,200 (EKARI 10,500)

Eneo hili ni mali ya Wizara ya Mifugo lipo kandokando ya Barabara kuu ya Songea – Njombe. Halmashauri ya Madaba inalitunza na kulitumia. Wawekezaji wanakaribishwa kwa ajili ya shughuli za ufugaji wa mifugo (Ng’ombe). Kwa sasa kuna wafugaji waliokodishwa vitalu 16. Hivyo bado kuna nafasi ya kupokea wafugaji wengine wanaohitaji kufuga kwenye vitalu 8. Aidha eneo limepitiwa na mto mkubwa unaowezesha kutumika kwa uzalishaji wa chakula (Nyasi) cha mifugo.

ENEO LA HALMASHAURI EKARI 500

Halmashauri inamiliki eneo lake la ekari 500 lililopo KM 18 kutoka barabara kuu ya Songea – Njombe ukielekea kijiji cha Ifinga. Eneo hili lipo tayari kwa Mwekezaji yeyote kuwekeza kwa shughuli za kilimo, hasa kilimo cha Miti, Kahawa na mazao mengine yanayoendana nayo.

MAPOROMOKO YA KUZALISHA UMEME WA MAJI

Halmashauri YA wilaya ya Madaba ina maporomoko yanayoweza kuzalisha umeme. Maporomoko haya ni pamoja na Masigira, Lipupuma na Lingatunda. Waekezaji wanakaribishwa kuwekeza.

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Chwaya atoa rai kwa walimu wa awali kutekeleza agizo la Serikali

    January 18, 2025
  • MARATIBU wa mradi wa BOOST Madaba amshukuru Rais Samia

    January 18, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa