• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

ZAIDI ya bilioni 2 zapitishwa bajeti 2023/2024 matengenezo ya Barabara Madaba

Posted on: February 13th, 2023

BARAZA la Madiwani Halmashauri ya Madaba limepitisha mpango wa bajeti  ya matengenezo ya Barabara  mwaka wa fedha 2023/2024 zaidi ya bilioni 2.

Kaimu Meneja  Wakala wa Barabara za Vijijini (TARURA) Wilaya ya Songea Godfrey  Mngale akisoma taarifa katika kikao cha Baraza la Madiwani amesema bajeti ya Mwaka 2022/2023 imetekelezwa na inaendelea kutekelezwa ikiwa mtandao wa barabara wenye jumla ya kilomita 629.7 ,kati ya hizo kilomita 196.31 za mjazo na 399.28 , za mkusanyo pamoja na 34.11 ni za jamii.

Mngale amesema hali ya Barabara katika Halmashauri hiyo kilomita 63 ambazo ni asilimia 10 ya barabara zina hali nzuri na kilomita 313 ambazo ni sawa na asilimia 49.7 zinahali ya kuridhisha  na 253.7 zinahali mbaya ambazo sawa na asilimia 40.28

Hata hivyo amesema katika Halmashauri ya Madaba imegawanyika katika makundi manne ambapo kilomita 38.870 ni barabara za changarawe,kilomita 5.55 ni barabara za lami na zege na kilomita 585.275 ni barabara za udongo.

“Katika mwaka wa fedha 2022/2023 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba ilitengewa zaidi ya milioni 2 kwaajili ya matengenezo ya mtandao wa barabara kutoka vyanzo vikuu  vitatu”.

Mngale amesema Mfuko wa Barabara uliidhinisha jumla ya shilingi milioni 638,mfuko mkuu wa Serikali kila jimbo la uchaguzi milioni 500, Serikali kupitia fedha za tozo bilioni moja.

“ Hadi kufikia Januari 2023 TARURA  imepokea kiasi cha  zaidi ya shilingi milioni 815 ambazo ni sawa na asilimia 37.46 ya bajeti”

Mhandisi amesema katika utekelezaji wa bajeti ya mwaka wa fedha 2022/2023 Halmashauri ya Madaba imetekeleza  jumla ya miradi 5 ikiwa na kilomita 24.81 zimefanyiwa matengenezo ya kawaida,kilomita 18.41 matengenezo katika maeeneo korofi,kilomita 7.37 matengenezo ya muda maalumu na makalavati 13 yametengenezwa kupitia mfuko wa jimbo.

Amesema jumla ya madaraja madogo 7 yanaendelea kujengwa kupitia fedha za tozo na jimbo la uchaguzi pamoja na ufunguzi wa barabara kilomita 53.12 kupitia fedha ya tozo ya mafuta hali ya matengenezo ya barabara Halmashauri ya madaba imefikia asilimia 52.16.

Imeandaliwa na Aneth Ndonde

Kutoka kitengo cha Mawasiliano Ofisi ya Mkurugenzi  Halmashauri ya Madaba

Februari,13,2023.

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • UJENZI WA MADARASA 2 NA MATUNDU 6 YA VYOO SHULE YA MSINGI KIPINGO WAKAMILIKA KWA ASILIMIA 100

    May 30, 2025
  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Chwaya atoa rai kwa walimu wa awali kutekeleza agizo la Serikali

    January 18, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa