• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

WAZIRI wa Maliasili na Utalii amewaagiza wananchi wa Mbangamawe Madaba kufanya shughuli zinazoendana na Uhifadhi

Posted on: April 29th, 2021

WAZIRI wa Maliasili na Utalii Damasi Ndumbaro  amewaagiza wananchi wa kijiji cha Mbangamawe Halmashauri ya Madaba mkoani Ruvuma kuweka matumizi sahihi yanayoendana na uhifadhi  wa  Maliasili  na Nyama pori.

Akizungumza katika mkutano wa Hadhara na wananchi hao amewaeleza faida  za Maliasili na wanyama pori ikiwemo ujenzi wa Barabara , Shule ,Vituo vya afya na Ajira watu zaidi ya  milioni 1  nchi nzima pamoja na kuleta fedha za kigeni dola bilioni 2.6.

“Usholoba ni mapito ya wanyama pori ,wanyama hao siyo wajinga wana hakili na wanakumbukumbu ndiomana Tembo akipita sehemu hata kama miaka 50 iliyopita atapita tena kwa sababu wanaishi kwenye familia na hakuna mtu anayeweza kuzaa na ndugu yake  na tembo wapo hivyo ,akitaka kuzaa anakwenda kwenye familia nyingine ndiomana wanapita kwenye hizi sholoba iliakazae watoto wazuri ni sababu za kisayansi”.

Hata hivyo amesema vijiji vitakuwepo na vitaendelea kuwepo na lazima wananchi watambue vimeanzisha kwenye usholoba na kinachotakiwa ni kuangalia kwenye mpango wa matumizi ya ardhi  na siyo kuwaonea wananchi.

“Njia za wanyama ni sawa na Mto huwezi kuzuia yakija nmafuriko huwezi kuzuia watakuja Tembo hapa mamia kwa mamia waue watu kwa faida ya Nani? Juzi tumesikia Jimbo la Tunduru Kusini kesi imekuwa ni Tembo kuua watu kwasababu kijiji kimeanzishwa kwenye usholoba na ni njia ya asili ya wanyama ilikuwepo na vijiji vimekuja na kukuta Usholoba upo”.

Waziri amewashukia  wenyeviti wa  vijiji na watendaji kuanzisha vijiji kwenye sholoba za wanyama ni kosa la viongozi hao kwasababu wanajua na baada ya kutatua tatizo wamekuwa wachochezi na kuwagombanisha wananchi na serikali yao.

Amesema Serikari ya Tanzania inawajali sana wananchi ndio maana imeleta  maendeleo nakuleta  umeme mpaka vijijini, na hawana mpango wa kubomoa nyumba ya mwananchini yeyote ilanikuweka matumizi sahihi ya ardhi na kuruhusu shughuli zinazoendana sambamba na uhifadhi ikiwemo kupanda miti na kufuga nyuki na ameahidi kuwaletea mizinga ya nyuki.

Mkuu wa Wilaya ya Songea Pololeti Mgema amesema kabla ya kutokea mgogoro huo walifanya mikutano ya kuwashirikisha wananchi hao ikiwemo uhifadhi wa Maliasili na wanyamapori unamanufaa mbalimbali ikiwemo mvua.

“Mimi niliwahi kufika hapa tulikaa masaa matatu na uongozi tukizungumzia habari la usholoba kila mtu alikuwa anazungumza lake wengine walidai hawajui usholoba,  nilipanga kufanya mkutano na kukubaliana wapi usholoba uanzie ili wananchi wasiendelee kufanya shughuli za kibinadamu kwenye eneno hilo na niliwapa kazi hiyo watu wa Maliasili na wanyama pori”.

Imeandaliwa na Aneth Ndonde

Afisa habari Halmashauri ya Madaba

Aprili 25,2021

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • UJENZI WA MADARASA 2 NA MATUNDU 6 YA VYOO SHULE YA MSINGI KIPINGO WAKAMILIKA KWA ASILIMIA 100

    May 30, 2025
  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Chwaya atoa rai kwa walimu wa awali kutekeleza agizo la Serikali

    January 18, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa