• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

WAZIRI wa Kilimo afunga maonyesho ya Mbolea Duniani Ruvuma

Posted on: October 14th, 2021

MAADHIMISHO ya siku Mbolea Duniani  yamefanyika kwa siku tatu katika uwanja wa Majimaji mjini Songea mkoani Ruvuma.

Maadhimisho hayo yalizinduliwa na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma  Brigedia Jenerali Wilberth IbugeOktoba 11  na  kufungwa na Waziri wa Kilimo Profesa Adolf Mkenda.

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali  Wiberth Ibuge akitoa salamu katika Maadhimisho hayo amesema juhudi za kisera kwenye kilimo zimesababisha Mkoa wa Ruvuma kuongoza kwa kuzalisha mazao ya chakula kwa miaka mitatu mfululizo.

RC Ibuge amelitaja suala la upatikanaji wa Mbolea  katika kilimo umeongezea tija na ufanisi wa uzalishaji wa Mazao hayo.

Hata hivyo amesema  kwa mwaka huu bei ya mbolea imepanda kutokana na kutegemea viwanda vya nje ya nchi hali ambayo inaleta changamoto kwa wakulima.

“Kilio chetu wanaruvuma na Watanzania wote tunatambua siyo serikali imesababisha bei ipande bali uzalishaji wa Mbolea tunategemea viwanda vya nje na Corona ilipo tupiga wazalishaji walifunga viwanda na walipofungua kila mtu Duniani anataka Mbolea bila shaka lazima bei ipande’’,alisema RC Ibuge.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Udhibiti Mbolea Tanzania TFRA  Profesa Antony Mshandete amesema idadi ya watu inatarajiwa kufikia bilioni 9.7 kufikia mwaka 2050 ambayo  itasaidia kuongezeka uchumi  wa viwanda na uhitaji wa kuzalisha mazao mengi kutoka katika eneo dogo.

Profesa Mshandete ameitaja kauli mbiu ya maadhimisho ya siku ya mbolea kwa mwaka 2021 kuwa ni Tumia Mbolea Bora kwa Tija na Kilimo Endelevu,ambapo amesema jukumu kuu ya TFRA  kupitia kaulimbiu hiyo ni kusimamia ubora wa Mbolea.

Hata hivyo amesema katika kutekeleza kauli mbiu hiyo TFRA imekuwa na mafanikio mengi  na kuendelea kuimarisha mifumo ya udhibiti wa Mbolea ili kuhakikisha wakulima wanapata Mbolea Bora kwa wakati wote.

“Mwaka 2016 hadi Septemba 2021 jumla ya mbolea zilizosajiliwa zilikuwa 356,Matumizi ya Mbolea yameongezeka uzalishaji mwaka 2015/2016 matumizi ya mbolea yalikuwa tani 296,036 na mwaka 2020/2021 matumizi ya mbolea yalikuwa 475,870”,alisema .

Hata hivyo  Profesa Mshandete ameyataja mafanikio ya TFRA kuwa ni kuendelea kuimarisha mifumo ya udhibiti wa Mbolea  ili kuhakikisha wakulima wanapata Mbolea bora,kuimarisha mfumo wa  utoaji  wa huduma za Mbolea ambapo hivi sasa huduma hutolewa kwa njia ya Mtandao.

Amezitaja changamoto za TFRA kuwa ni gharama za upatikanaji wa malighafi za kutengenezea Urea,Matumizi madogo ya Mbolea, Huduma isiyotoshelevu ya ugani,bei kubwa za Mbolea  hasa katika soko la Kimataifa na Mabadiliko ya tabia ya Nchi ambayo yanayumbisha kwa Masoko.

Habari imeandikwa na Mwandishi wetu

Ruvuma

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Chwaya atoa rai kwa walimu wa awali kutekeleza agizo la Serikali

    January 18, 2025
  • MARATIBU wa mradi wa BOOST Madaba amshukuru Rais Samia

    January 18, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa