• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

WAZIRI Mkumbo ampongeza mwekezaji Silver Land Ndolela kwa kilimo cha Mbegu Madaba

Posted on: August 23rd, 2023

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji Profesa Kitila Mkumbo ametembelea eneo la uwekezaji  wa Mbegu shamba la Silver land Ndolela  lenye Hekta 5000  Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.

Akizungumza mara baada ya kukagua eneo hilo amesema wawekezaji hao wanazalisha mbegu za aina nne ikiwemo Maharage,Viazi,Ngano na Mahindi.

Mkumbo amesema katika Nchi ya Tanzania moja ya changamoto ya Kilimo ni mbegu ambazo zinatumiwa kwa mda mrefu na kupelekea kulima eneo kubwa na kuvuna kidogo hivyo uwepo wa wawekezaji hao utapelekea kutatua changamoto uhaba wa Mbegu.

“Mara nyingi Waziri wa Kilimo amesema changamoto za Kilimo ni swala la Mbegu na Mbolea hayo ni maeneo makubwa yanayosumbua uwepo wa wawekezaji hao ni msaada mkubwa ambao wamewekeza katika Halmashauri ya Madaba”.

Hata hivyo Mkumbo amepokea changamoto wanayokutananayo wawekezaji hao ikiwemo swala la chokaa ambayo wanaagiza kutoka Mkoa wa Tanga kwaajili ya  kuchanganya kwenye ardhi ya Ruvuma kwasababu ina acidi.

Amesema Wilaya ya Songea ina chokaa watahakikisha Serikali inatafuta wawekezaji kwaajili ya kuchakata chokaa ili wananchi wa Ruvuma waweze kutumia Chokaa inayopatikana ndani ya Mkoa na itawasaidia kupunguza gharama za matumizi makubwa ya Mbolea

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Songea Wilman Ndile katika ziara hiyo amesema Waziri Kitila Mkumbo amejionea uwekezaji huo ikiwa wawekezaji wengi kuwekeza katika viwanda na kukwepa kuwekeza kwenye kilimo.

Amesema Wawekezaji wa Silver land Ndolela wameamua kuwekeza katika kilimo ikiwa Wilaya ya Songea  kuna wawekezaji wawili akiwemo Avivu amewekeza katika kilimo cha Kahawa na Silver Land Ndolela amewekeza katika Mazao ya chakula.

Imeandaliwa na Aneth Ndonde

Kutoka Kitengo cha Mawasiliano Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

Agosti 23,2023.

 

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Chwaya atoa rai kwa walimu wa awali kutekeleza agizo la Serikali

    January 18, 2025
  • MARATIBU wa mradi wa BOOST Madaba amshukuru Rais Samia

    January 18, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa