• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

WATUMISHI Madaba wajitokeza kupata kinga tiba ya Usubi

Posted on: August 22nd, 2023

WATUMISHI Halmashauri ya Wilaya ya Madaba  wemejitokeza kupata kinga tiba ya  Usubi  wakiongozwa na kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Maternus Ndumbaro ambae ni Mkuu wa Idara ya Elimu Sekondari.

Zoezi hilo limefanyika Katikan ukumbi wa Halmashauri na wemepewa Elimu ya ugonjwa huo unaoathiri ngozi na macho na kusababishwa na minyoo iitwayo (Onchocerca  Volvulus).

Mratibu wa Magonjwa yasiyopewa kipaumbele  Halmashauri ya Madaba Dokta Betty Mbawala amesema Minyoo hiyo huenezwa na inzi weusi wadogo wanaozaliana kandokando ya mito yenye maji yanayoenda kwa kasi.

Mratibu wa Magonjwa hayo  amezitaja dalili za ugonjwa huo ikiwemo maambukizi ya vimelea vya usubi vinavyosababisha na  kuwasha kwa ngozi,ukurutu usiotibika,kuwa mithili ya ngozi ya kenge au Mamba,kuwa na vinundu sehemu ya mifupa pamoja na kuwa na ngozi yenye mabaka mithili ya mtu aliyeungua na moto au kama ngozi ya chui.

Hata hivyo Mratibu amewakumbusha wananchi mara wanapoona dalili hizo wawahi kituo cha kutolea huduma  za Afya kwa uchunguzi  na matibabu zaidi.

Mbawala ameyasema madhara yanayoweza kutokana na ugonjwa wa Usubi  ikiwa pamoja na ngozi kuharibika, kutoana vizuri na kupelekea upofu wa macho, kushindwa kufanya kazi kupelekea umaskini na utegemezi katika Familia.

“Ugonjwa wa Usubi unazuilika kwa kumeza kinga tiba kwa kila mtu kuanzia umri wa miaka mitano kila zinapotolewa kwenye jamii”.

Imeandaliwa na Aneth Ndonde

Kutoka kitengo cha Mawasiliano Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

Agosti 22,2023.

 

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Chwaya atoa rai kwa walimu wa awali kutekeleza agizo la Serikali

    January 18, 2025
  • MARATIBU wa mradi wa BOOST Madaba amshukuru Rais Samia

    January 18, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa