• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

WATENDAJI wa AMCOS wapata mafunzo ya uandaaji wa vitabu na Mbinu za kupata hati safi

Posted on: September 21st, 2021

KATIBU Tawala msaidizi Uzalishaji na Uchumi Mkoa wa Ruvuma Jeremia Sendoro amefungua mafunzo ya uandaaji wa vitabu na Mbinu za kupata hati safi kwa wahasibu na waandishi wa AMCOS kanda ya Kusini.

Akizungumza katika ufunguzi wa Mafunzo hayo  amesema Mafunzo ya wahasibu na waandishi wa vyama vya Ushirika wa Mazao na Masoko (AMCOS)  yamejumuisha mikoa ya Lindindi,Mtwara, Ruvuma na Mbeya  na kufanyika katika ukumbi wa SUT SACCOS Manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma.

“Elimu na Mafunzo ni moja kati ya Misingi saba ya Ushirika ya Kimataifa, hivyo mafunzo ni utekelezaji  wa msingi katika kuimarisha vyama vya ushirika kwa lengo la kuvifanya  vyama kuwa na hati safi “.

Sendoro amesema Ushirika utakuwa na maana kwa Taifa ikiwa utaongeza uzalishaji na kurahisisha masoko ya Uhakika ya mazao,na hatimaye kushinda vita dhidi ya umaskini.

“Naomba niwakumbusheni kuwa ushirika ni dhana muhimu ya kujenga uchumi imara na wenye nguvu katika kupunguza na kama si kuondokana kabisa  na mfumo wa ushirika ni mfumo pekee na muhimu wa kupambana  na vita dhidi ya uchumi”.

Sendoro amesema Serikali inatambua,Ushirika ni dhana pekee ya kumkomboa mkulima na mnyonge kiuchumi ,Ushirika umeelekezwa katika ilani ya utekelezaji wa chama cha Mapinduzi (CCM) ya  mwaka 2020 hadi 2025 kuwa ni nyenzo muhimu ya kukuza Uchumi.

Katibu Tawala msaidizi ametoa wito  kwa viongozi na watendaji wa vyama vya Ushirika kuwa karibu na wakulima wakati wote wa shughuli za msimu ili kubaini na kutatua changamoto mbalimbali za utekelezaji  wa shughuli za masoko,kusimamia na kuhakikisha wakulima wote wanauza mazao kupitia mifumo iliyoelekezwa na Serikali.

Kwa upande wake Afisa mipango Emmanuel  Danda amesema kuwa changamoto zinazosababisha  wanachama kupata hati chafu  ni elimu katika eneo la uhasibu kupelekea   kuwa na hati chafu kwa vyama vya ushirika.

Danda amesema kwa msimu huu na ujao wamejipanga kwa kutafuta wadau ili waweze kuimarisha masoko na kuwajengea uwezo watendaji ili mifumo ya vyama vya ushirika iweze kufanya vizuri kwa wakulima.

Mwenyekiti wa Mafunzo hayo Hamza Rashi Mbutuka akisoma Risala kwa mgeni rasmi amewapongeza waandaji wa mafunzo ambao ni wakufunzi kutoka chuo cha Ushirika Moshi,Chuo cha uhasibu na maafisa ushirika kutoka Wilaya mbalimbali zilizomo ndani ya Mkoa na nje ya Mkoa.

Imeandaliwa na Aneth Ndonde

Kutoka ofisi ya Habari Mkoa wa Ruvuma

Septemba 21,2021.

 

 

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MADABA YAPONGEZWA KWA KUPATA HATI SAFI KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    June 19, 2025
  • UJENZI WA MADARASA 2 NA MATUNDU 6 YA VYOO SHULE YA MSINGI KIPINGO WAKAMILIKA KWA ASILIMIA 100

    May 30, 2025
  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa