• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

WANANCHI Madaba wamshukuru Rais Samia kwa kutoa fedha za ujenzi wa Soko la Kihistoria

Posted on: September 13th, 2023

MWENYEKITI wa Kijiji cha Lituta Halmashauri ya Madaba Beno Mwenda ameishukuru Serikali kwa kutoa fedha shilingi Milioni 190  kwaajili ya ujenzi wa Soko la Kihistoria.

Mwenda amesema katika Halmashauri hiyo  haijawahi kutokea tangia kuanzishwa kwa Halmashauri hiyo kupata Soko la kisasa ambalo litapelekea Wajasiriamali kufanya biashara zao katika mazingira rafiki.

Kwa upande wa Mtendaji wa Kijiji cha Lituta Aisha Nyange akisoma taarifa ya ujenzi wa Soko hilo linalojumuisha matundu ya Vyoo 6,Guba na Vizimba amesema kijiji hicho kimeanza kutekeleza  mpango wa kunusuru kaya maskini (TASAF)  awamu ya tatu mwaka 2015 ambapo utekelezaji wake ulifanyika kupitia Halmashauri ya Songea.

Nyange amesema Octoba 2022 Wananchi wa Kijiji cha Lituta walifanikiwa kuibua mradi wa ujenzi wa Soko na mchako wa makadirio ya bajeti ulifanyika kwa kwa kushirikiana na wataalamu ngazi ya Halmashauri na kupokea kiasi cha zaidi ya shilingi Milioni 190.

Amesema matarajio ya wananchi baada ya kupokea fedha za utekelezaji wa Mradi huo utakapo kamilika  kupanua wigo wa bidhaa,kupunguza  gharama kwa wananchi kwenda kutafuta mahitaji katika Wilaya za jira, Kuongeza mapato katika kijiji na Halmashauri.

“Tunatoa shukrani za dhati kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kwa kutupatia fedha kwaajili ya ujenzi wa Soko  la kisasa katika Halmashauri yetu”.

Kutoka kitengo cha Mawasiliano Halmashauri ya Madaba

Septemba 13,2023.

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Chwaya atoa rai kwa walimu wa awali kutekeleza agizo la Serikali

    January 18, 2025
  • MARATIBU wa mradi wa BOOST Madaba amshukuru Rais Samia

    January 18, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa