• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

WALIMU wapewa mikakati ya uboreshaji Elimu 2023

Posted on: January 25th, 2023

TIMU ya Maafisa  Elimu wa  Halmashauri ya  Madaba imefanya  kikao kazi  na walimu Msingi na Sekondari pamoja na  Maafisa Elimu Kata katika Kata 5 kwa lengo la kuweka mikakati ya Kitaifa ya uboreshaji wa Elimu.

Mkuu wa Idara ya Elimu Msingi Katika Halmashauri hiyo Saada Chwaya katika ziara hiyo ya kikao kazi amezungumza na Walimu wa Kata hizo ikiwemo Mtyangimbole,Ngumbiro,Mkongotema,Lituta na Mahanje kwa  kuwajuza mikakati ya Kitaifa ya Elimu iliyowekwa kwaajili ya utekelezaji  kuanzia Januari  2023  hadi Desemba 2023.

“Tumena matokeo ya Darasa la Nne,Darasa la Saba pamoja na Kidato cha Nne na tumeona wapi tulijikwaa ili mwaka huu 2023 tusijikwae tena “.

Chwaya ametoa rai kwa Walimu wahakikishe wanatekeleza mikakati iliyowekwa Kitaifa  ili kuhakikisha Madaba inafanya vizuri kimkoa na Kitaifa kwa upande wa Elimu Msingi na Sekondari.

Teddy Sanga akisoma mikakati hiyo kwa Wakuu wa Shule Msingi na Sekondari amesema  asilimia 100  kila mwalimu afanye tathimini ya matokeo ya upimaji wa maatokeo ya kitaifa  ndani ya siku saba baada ya matokeo.

Amesema  mikakati itakayo mwezesha  kila mwalimu wa Sekondari na Msingi kufanya ufuatiliaji na tathimini ya ufundishaji na ujifunzaji kwa wanafunzi darasani kila mmoja na somo lake kwa majaribio ya wiki,mwezi,robo,robo tatu hadi mwaka kama wanapanda au wanashuka.

“Kila mwalimu wa Shule ya Msingi au Sekondari ahakikishe anampango kazi  wa Utekelezaji na miongozo ya Kielimu ya Halmashauri na Shule kwa muhula wa kwanza wa masomo mpango kazi ndio dira”.

Hata hivyo Sanga amesema kwa upande wa Shule ya Msingi mwalimu ahakikishe asilimia ya mwanafunzi wa darasa la pili aweze kumudu  stadi za kusoma afikapo Machi 30,kila mwaka kwa kusoma na kuheshabu.

Kwa upande wake Afisa utumishi wa Halmashauri hiyo Hope Challe amewakumbusha Walimu wajibu wao wawapo eneo la kazi  pamoja na kuwachukulia wanafunzi ambao hawana uelewa wa haraka pamoja na kuto wanyanyapaa.

Challe amewakumbusha walimu kuepuka rushwa eidha kutoka kwa wazazi au watu wengine na kuwapelekea kupata changamoto ya kufukuzwa kazi, au kushushwa daraja pamoja na kufuata taratibu,miongozo na kanuni iliyowekwa na Serikali.

Afisa utumishi ametoa rai kwa walimu hao kuhakikisha wanawashirikisha wananchi miradi inayoletwa na Serikili na inayojengwa katika eneo lao ili wajue Serikali imeleta fedha kwaajili ya miradi ya maendeleo.

Imeandaliwa na Aneth Ndonde 

Kutoka Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Madaba

Januari 25,2023. 

 

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MADABA YAPONGEZWA KWA KUPATA HATI SAFI KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    June 19, 2025
  • UJENZI WA MADARASA 2 NA MATUNDU 6 YA VYOO SHULE YA MSINGI KIPINGO WAKAMILIKA KWA ASILIMIA 100

    May 30, 2025
  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa