• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

WALIMU Madaba wapewa Mafunzo ya Mtaala ulioboreshwa

Posted on: January 11th, 2024

WALIMU wa Awali na Msingi Halmashauri ya Wilaya ya Madaba Mkoa wa Ruvuma wamepewa mafunzo ya Mitaala iliyoboreshwa.

 Afisa Elimu Kata ya Mahanje Ruthness Mbuba akizungumza katika mafunzo hayo amesema  lengo la kufanya mafunzo hayo kwa Walimu ni kuwajengea uwezo ili waweze kwenda na mabadiliko ya Mtaala ulioboreshwa wa mwaka 2023.

“Mtaala huu tunaanza kuutumia mwaka 2024 na unalenga darasa la awali,la kwanza na darasa la tatu na tunatarajia baada ya mafunzo haya walimu watatekeleza kwa kutumia mbinu mpya katika ufundishaji”.

Naye Afisa Elimu Elimu Maalumu Teddy Sanga akimwakilisha Afisa Elimu wa Halmashauri  hiyo Saada Chwaya katika Mafunzo haya amesema katika mtaala huo walimu wasisahau watoto wenye mahitaji maalumu.

“Watoto wenye mahitaji maalumu siyo tu wale waliopo shuleni hata waliofichwa nyumbani walimu wenzangu tuwatumie viongozi wamaeneo hayo kama kuna watoto waliofikia umri wa kwenda shule lakini hawajaandikishwa waanze shule”.

Hata hivyo Sanga amewapongeza walimu katika Kata zote kwa kushiriki Mafunzo hayo ambayo yatasaidia kuboresha ufundishaji kwa watoto.

“Mafunzo haya yanakwenda kuboresha ufundishaji wetu kwa watoto  ili tuweze kuendana na dunia ya Sayansi na Teknolojia kwa kupata vitu vipya na namna ya kuwafundisha”.

Kutoka Kitengo cha Mawasiliano Halmshauri ya Wilaya ya Madaba

Januari 11,2024.

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Chwaya atoa rai kwa walimu wa awali kutekeleza agizo la Serikali

    January 18, 2025
  • MARATIBU wa mradi wa BOOST Madaba amshukuru Rais Samia

    January 18, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa