• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

WAKALA wa Vipimo Ruvuma watoa mafunzo kwa wadau wa biashara

Posted on: May 5th, 2021

KAIMU MKUU wa Mkoa wa Ruvuma Pololeti Mgema amefungua Semina inayolenga kuongeza Uelewa wa Matumizi ya Vipimo sahihi Ruvuma.

Akizungumza katika Semina hiyo amesema ni semina iliyolenga makundi mbalimbali ikiwemo Wakulima,Wajasiliamali,Viongozi wa Masoko,Wasindikaji wa Unga,na wafanyabiaashara wa Jumla.

“Natoa shukrani zangu za pekee kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kujenga mazingira bora ya ufanyaji wa Biashara ya Mazao na kuendelea kusisitiza utumiaji wa Vipimo sahihi ili kuleta tija na usawa kwa Mkulima ”.

Hata hivyo Mgema amesema ni mwendelezo wa utekelezaji wa Wakala wa Vipimo kwa jamii na kutoa Elimu kwa wadau kupitia Television(TV)Magazeti,Radio pamoja na Mikutano mbalimbali.

Amesema kumekuwa na matumizi makubwa ya Vipimo batili katika maeneo ya Biasharahususani kwenye Masoko ya Manispaa na Wilaya na watu wamekuwa wakitumia Vipimo visivyo rasmi vinavyojulikana kama makopo,dumla,ndoo na lita.

“Katika Ilani yetu ya CCM ya chama cha Mapinduzi ya mwaka 2020-2025 ibara ya 37B(d,f,g,h) ina sisitiza uongezaji wa tija na faida katika shughuli za wakulima ili kuongeza uzalishaji”.

Pia Mgema ameipongeza Taasisi ya Wakala wa Vipimo kwa kuanzisha maeneo mapya ya ukaguzi ilikupanua wigo wa kumlinda mlaji kutokana na matumizi sahihi ya Vipimimo.

Kaimu Meneja wa Wakala wa Vipimo Nyagabona Mkanjabi katika semina hiyo  amesema kwa Mkoa wa Ruvuma matumizi ya Vipimo sahihi yapo china sana kwa wafanyabiashara ishara inayoonesha bado hawajahamasika kutumia vipimo sahihi.

Mkanjabi amewaomba wafanyabiashara kuanza kutumia ili wanchi wafuate matumizi ya makopo siyo sahihi

“Wafanyabiashara kutumia makopo na kuamini jamii haikubari bado siyo sahihi kwa sababu hao wanaolalamika wanaenda Buchani ananunua nyama inayopimwa kwenye mzani,Sukari ananunua kwa kupimwa kwenye mzani ni utamaduni ambao watu wamejijengea pamoja na wateja wao kutumia makopo kwa namna nyingine wanajinufaisha wafanyabiashara na kuwapunja wateja”.

Imeandaliwa na Aneth Ndonde

Afisa habari Halmashauri ya Madaba

Mei 5 ,2021

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Chwaya atoa rai kwa walimu wa awali kutekeleza agizo la Serikali

    January 18, 2025
  • MARATIBU wa mradi wa BOOST Madaba amshukuru Rais Samia

    January 18, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa