• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

WAGONJWA 692 wapata huduma kituo cha afya Matetereka

Posted on: July 16th, 2024

KITUO cha afya Matetereka Halmashauri ya Wilaya ya Madaba kilichojengwa kwa zaidi ya shilingi bilioni moja kimeanza kutoa huduma.

Hayo amesema mganga Mfawidhi wa kituo hicho Yusuph Mnazi katika ziara ya Mbunge wa Jimbo la Madaba  Joseph Mhagama kuwa hadi kufikia sasa wagonjwa 275 wamepata huduma katika kituo hicho,wagonjwa wa marudio 380,wanawake wajawazito 10,huduma ya uzazi wa mpango kwa akinamama na akina baba 27.

“Serikali imeleta vifaa tiba ambavyo mda si mrefu vitaanza kutumika na huduma itakayopatikana itakuwa ni bora na bobezi”.

Diwani wa Kata hiyo Hamfrey Mwenda amesema ujenzi wa Kituo hicho cha afya Matetereka kilijengwa  kwa shilingi milioni 562  kwa mradi wa tozo mwaka 2021/2022 Milioni 500 ililetwa kwa awamu ya mbili,na mapato ya ndani ya Halmashauri ilitoa kiasi cha shilingi Milioni 62 kwa awamu mbili tofauti ikiwa Mwaka 2022/2023 ilitoa Milioni 42, Mwaka 2023/2024 ilitoa milioni 20.

Hata hivyo ujenzi huo unahusisha majengo manne  OPD,mama na mtoto, maabara na jengo la kufulia pamoja na kichomea taka majengo hayo yamefikia hatua ya ukamilishaji na kuanza kutoa huduma.

Mwenda ametoa shukrani kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan na Mbunge wa Jimbo la Madaba Joseph Mhagama kwa kuleta fedha kwaajili ya ujenzi wa Kituo cha afya.

Imeandaliwa na Aneth Ndonde

Kutoka Kitengo cha Mawasiliano Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

Julai 15,2024.

 

 

Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Chwaya atoa rai kwa walimu wa awali kutekeleza agizo la Serikali

    January 18, 2025
  • MARATIBU wa mradi wa BOOST Madaba amshukuru Rais Samia

    January 18, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa